KIUNGO wa
mabingwa wa England, Manchester City, Yaya Toure amesema anataka
kubakia klabuni hapo kwa muda mrefu kadiri itakavyowezekana.
Nyota
huyo mwenye miaka 31 mapema mwaka huu aliripotiwa kutimka Etihad baada
ya wakala wake, Dimitri Seluk kusema kuwa Toure alijisikia kutothaminiwa
na klabu baada ya kutotumiwa salamu za siku ya kuzaliwa mwezi mei.
Toure mwenye alieleza kuwa anavutiwa kujiunga na matajiri wa Ufaransa, Paris Saint-Germain.
Siku za
nyuma Toure alisema kwamba, mashabiki wasisikilize maneno ambayo
hayajatoka mdomoni mwake, lakini kila asemacho Dimitri ni sahihi
kwasababu anazungumza kwa niaba yake, ingawa kwasasa anasisitiza kuwa
wakati wote amekuwa kimya kuhusu furaha yake na hatima yake ya baadaye.
No comments:
Post a Comment