
Mwanafunzi mmoja amesema kwamba yeye na wenzake walifuata maagizo hayo hadi pale mlango wa chumba chao ulipokuwa juu ya vichwa vyao huku maji yakiingia ndani ya feri hiyo kupitia madirishani.
Mwengine alitaka kujua ni kwa nini waokoaji hawakuingia ndani ya chombo hicho ili kuwasaidia kutoka.
Wanafunzi walikaribia kwenye milango ya kutoka ambapo walisaidiwa kutoka na wanafunzi wenzao.
Feri hii ilizama tarehe kumi na sita mwezi wa Aprili kwenye kisiwa cha Jeju ambapo watu mia tatu na wanne waliaga dunia.
Wanafunzi hao walikuwa wakitoa ushahidi katika kesi wanohukumiwa wafanyikazi wa feri hiyo.

Wanafunzi wananza kutoa ushahidi Korea
Wengi wa Walioaga dunia kwenye meli hiyo ya Sowel walikuwa wanafunzi kutoka shule moja ya upili waliokuwa kwenye ziara ya shule.
Wafanyikazi wanashtumiwa kwa kosa la kutomakinika na kutelekeza majukumu yao .
Nahodha na maafisa watatu pia wanakabiliwa na kosa la mauaji kwa njia ya uzembe kwa makusudi.

Hata hivyo waendeshaji mashtaka walisema kuwa tendo la nahodha na wafanyikazi kuwaagiza abiria kutulia humo ndani feri hiyo ilipokuwa ikizama kulisababisha vifo zaidi.
Jumatatu ilikuwa siku ya kwanza wanafunzi hao walikuwa wanatoa ushahidi .
Baadhi ya wanafunzi walionusurika
Msichana mmoja alisema kuwa Kulikuwa na wanafunzi wengi katika ukanda wa meli ambao walizuiliwa kwenye feri hiyo.
Mkasa huu ulisababisha hasira nchini Korea Kusini ikiwemo ukosoaji mkali kwa wafanyikazi wa serikali na wanabiashara ambao wanasemekana kutowajibika katika kazi yao ama pia yawezekana ufisadi ulipelekea mkasa huo.
Mwaanzoni mwa mwezi huu,polisi walitambua maiti ya mwenye kampuni inayomilika meli hiyo Yoo Byungeun .
Mwanawe wa kiume Yoo Dae-Kyun alikamatwa ijumaa.
No comments:
Post a Comment