Thursday, 24 July 2014

Mambo kumi husiyo yajua kuhusu Samuel Eto'o

 STAR anayetokea pande za Cameroon Samuel Eto’o ambaye anajulikana sana katika bara la Afrika kama msakata kabumbu bora kwa muda wote,Eto’o ambaye ametengeneza jina kupitia ligi aliyokuwa akichezea ya La Liga  Spain. Hungana na mimi katika kukuletea mambo kumi husiyo yajua kuhusu Samuel Eto’o mwanasoka bora wa muda wote barani Afrika.
ETO'O MCHEZAJI BORA KUTOKEA KATIKA ARDHI YA CAMEROON.
Japokuwa Eto’o hakushiriki kikamilifu katika kombe la dunia lilofanyika Brazili kwa kuwa alikuwa anauguza maumivu yakifundo cha mguu lakini atabakia kuwa katika wachezaji bora kuwai kutokea katika ardhi ya Cameroon.
Hata hivyo bado Eto’o ni mchezaji ambaye anamchango mkubwa katika klabu yake ya Chelsea ambayo inashiriki katika ligi kuu ya Uingereza ambayo inaushindani mkubwa balani ulaya.

ETO'O AJULIKANA KAMA  “Roger Milla” MDOGO KIPINDI ANACHIPUKIA KISOKA.
Kwa kipaji alichokuwa nacho kipindi ambacho anaanza kusakata kabumbu wapenzi wa kandanda nchini Cameroon waka mfananisha na Nguli wa kabumbu Cameroon na barani Afrika wakamwita “Little Milla”.
Sababu nyingine za kumwita “Little Milla” pale alipokuwa anapenda kuvaa jezi yenye jina la Nguli huyo katika mechi alizokuwa akishiriki akiwa mdogo na kulitendea haki akiwa uwanjani kwa kuonyesha vitu adimu kupelekea kupewa jina hilo.
Moja ya mjadala uliowahi kutokea  BBC kuhusu kipaji cha Eto’o na kikifananishwa na Roger Milla na kukili kuwa anastaili kubeba jina hilo kubwa barani Afrika ndipo mmoja wa wachambuzi alisema “Siyo mchezaji bora Afrika pekee bali alistahili kuwa  mmoja wa wachezaji bora katika mashindano ya kombe la dunia 2006,lakini kati yetu hatufikilii hilo labda kwakuwa yeye anatokea Afrika.” na kuongeaza kuwa lakini kupewa jina hilo ni heshima tosha nalinaleta amasa.
ETO'O ALISHAWAI KUKATALIWA KATIKA KLABU ZINAZOFUNDISHA SOKA KWA WATOTO UFARANSA ALIPOKUWA MTOTO.
Kipindi alipokuwa mototo Eto’o hakuweza kujiunga na klabu zinazofundisha soka Ufaransa kutokana na tatizo la kitambulisho cha uraia badala yake akatimkia katika klabu ya watoto ya Real Madrid  na kufanikiwa kuwa moja wanafunzi katika kituo hicho mwaka 1997 na kufanikiwa kucheza kwa mkopo katika klabu tofauti zinazo cheza katika ligi kuu miaka ya 1990’s.  
KWA MARA YA KWANZA AKIWA MCHEZAJI WA KULIPWA ANAFANIKIWA KUPELEKA NYUMBANI KIASI CHA DOLA 200 KATIKA MSHAHALA WAKE WA WIKI. 
Kipindi Eto’o anaanza kulipwa alikuwa pokea zaidi ya dola za kimarekani 200 kwa wiki kitu ambacho familia yake ilijivunia na katika mahojiano yake alishawai kusema kuwa Baba yake alishawahi kumuhuliza kuwa” kumbe unaweza kupata pesa nyingi kupitia mchezo wa mpira?”Eto’o akaongeza kuwa kutokana na amasa hiyo kutoka kwa Baba yake akajikuta baadae anapesa nyingi kwa kufanya vizuri katika kusakata kabumbu.
HATIMAYE ETO'O ANAMILIKI PASSPORT YA SPAIN AKIWA MCHEZAJI WA KULIPWA.
Baada ya kusota na kutumia muda mwingi akiwa katika soka la spaini  hatimaye Eto’o anafanikiwa kuwa na passport ya nchi hiyo.
Kitambulishi hicho “passport”itamuwezesha kutambulika kama sehemu ya Raia wa nchi hiyo na kumuwezehsa kufanya kazi katika nchi zote zilizopo jumuiya ya ulaya.

SAMUEL ETO'O AFANIKIWA KUMUOA MKEWE GEORGETTE 2007.
 June 2007, Eto’o anafunga ndoa na rafiki yake wa kike wa muda mrefu Georgette na upendelea kwenda kujirusha mara kwa mara wanapopata muda jijini Paris wakiwa na watoto wao watatu Etienne,Melle na Siena.
Eto’o anarecord ya kuwa  mchezaji wa kwanza kutoka Afrika kucheza mara nyingi katika ligi kuu ya spain.
Kipindi kirefu Eto’o ametumia muda wake akichezea ligi ya La liga akiwa  mchezaji wa Real Madrid  ambapo akitolewa kwa mkopo katika klabu za Leganes pamoja na Espanyol na nyingine nyingi uwezi kuisahau klabu ya Mallorca akitumia misimu minne na hatimaye akatua katika viwanja vya nou camp Barcelona na kufanukiwa kufunga magoli 108 akicheza mara 108.
ETO'O ANATAMBULIKA MCHEZAJI BORA WA MUDA WOTE AFRIKA

Eto’o amefanikiwa kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika 2003,2004,2005 na 2010 pia amefanikiwa kuwa mchezaji bora wa dunia 2005 akiwa nafasi ya tatu katika tuzo zilizotolewa na FIFA za( runner up for FIFA wourld Player year 2005) kipindi hicho wapenzi wengi wa mpira walidai Eto’o alistaili kuwa katika nafasi ya kwanza labda kwa  kuwa alikuwa anatokea Afrika.
Ni mmoja ya washindi wa tuzo ya Gold medal 2000 akiwa na timu yake ya Cameroon katika mashindano ya Olympic vilevile akiwa na timu yake ya Taaifa ya Cameroon amefanikiwa kuchukua mara mbili mashindano ya mabingwa wa mataifa ya Afrika.
Eto’o anajulikana mpachika mabao wa muda wote katika ardhi ya Cameroon na mchezaji wa tatu kutokea katika Historia ya nchi hiyo.
ETO'O ALISHAWAI KUOGELEA MAJI YA MOTO WAKATI BARCELONA WALIPOSHINDA KOMBE LA LIGA 2004-05
Baada ya Barcelana kushinda klabu bingwa ulaya 2005 na kupelekea kufanya sherehe katika uwanja wa Camp Nou  huku Eto’o akiwadhiaki mashabiki wa Mdrid kuwa ni wajinga heshima kwa mabinwa, “Madrid, carbon, Saluda al campeón”akimaanisha kwa lugha ya kingereza kuwa “Madrid, bastards, salute the champions.” ambapo kwa kipindi hicho Eto’o alikuwa Barcelona na pia walikuwa mabingwa ikapelekea uongozi wa klabu yake wamtake kuomba ladhi kwa Madrid kwa kuwa ndiyo klabu ya kwanza iliyomlea.
ETO'O ALISHAWAI KUANDIKA VITABU NANE JUU YA MAISHA YAKE.
Katika kitabu chake cha mwisho  ambacho kinasema  Bingwa kazaliwa “Birth of Champion” kinaelezea sana maisha ya key a Utoto tangia akiwa  Doula Cameroon.Joel  Esso akijulikana katika kitabu hicho ambaye amevaa uhusika wa Eto’o.
Eto’o alipotakiwa kueleza sababu za yeye kuandika kitabu hiki alisema kuwa nataka kutumia lugha ya watoto kwa sababu wao ni kizazi kinachofuata baada ya sisi na wao pia ni kizazi kinacho tuwakilisha sisi sote pia naitaji kuwasiliana nao kwa lugha yao.
“Naitaji kutumia lugha ya watoto kwa kuwa wao ni kizazi kijacho pia wanatuwakilisha sisi sote”alisema Eto’o katika mahojiano yake.

ETO'O AJENGA SHULE ZA KUKUZA VIPAJI VYA SOKA AFRIKA.
Katika kusaidia vipaji vya soka Afrika Eto’o akaanzisha Eto’o’s foundation ambayo inahusika na mipango
Katika Eto’o’o foundation imefanikiwa kuwa na shule za kukuza vipaji nchini Gabon pamoja na Nairobi Kenya kama sehemu ya mpango huo huku akisema naitaji kurudisha fadhira kwa Afrika.
“Nataka kurudisha shukrani kwa  Afrika  katika kipindi changu cha kucheza mpira na kunifanya kuwa bora  ”alisema Eto’o


No comments:

Post a Comment