Monday, 14 July 2014

CHRISTINA:Sera ya madaftari saba kwa wanafunzi wa darasa kwanza sio njia ya kukwamua elimu ya msingi



MFUMO  mbovu wa elimu  nchini bado ni tatizo  kwa shule za msingi na Sekondari katika kuleta mabadiliko yanayotarajiwa na Sera ya Elimu, matokeo makubwa sasa(BRN), kama mpango wa wizara unavyo sema.
Ingawa serikali imekuwa ikibuni mipango mbalimbali ya kuboresha Elimu kama mpango huu wa matokeo makubwa sasa (BRN) lakini bado ipo haja kwa wizara  ya elimu kujitathimini upya ili kufanya maboresho katika Sera yake kwa kuwa ni tatizo kubwa kwa shule za msingi.
Inaelezwa kuwa mabadiliko ya mara kwa mara ya Sera ya Elimu yamechangia wanafunzi wengi kushindwa kusoma na kuandika kutokana na mfumo wa Elimu ulivyo unao mtaka  mtoto wa darasa la kwanza asome masomo saba badala ya  matatu.
Tangu  Wizara ya Elimu ilipo badilisha Sera ya elimu inayomtaka mwanafunzi wa darasa la kwanza na darasa la pili kusoma masomo saba badala ya matatu kama ilivyokuwa mwanzo imepekelekea uelewa mdogo kwa wanafunzi.
 Hata hivyo, kinyume na matarajio  uamuzi  huo haukuweza kuleta matunda mazuri badala yake umepoteza uwezo wa mtoto wa kusoma na kuandika kwakumpa mtoto mzigo mkubwa.
Mavuno ya uwamuzi huo hasi,ndio unafanya leo hii  ni jambo la kawaida kumkuta mtoto wa darasa la saba anamaliza shule hawezi kusoma wala kuandika kwa ufasaha na inapelekea msingi wake wa elimu  kuwa mbovu.
Mwelekeo huo unawatia hofu wadau mbalimbali wa Elimu nchini wakiwemo walimu , wazazi na wanaharakati wakidai kuwa mfumo huo wa Elimu bado utaendelea kuzalisha mbumbu wasio jua kusoma na kuandika kama hautobadilishwa.
Mwalimu  Stanley  Muhimbula, ni mwenyekiti wa taaluma katika shule ya msingi Bunge ,anasema kuwa mtoto mdogo inabidi ajifunze kulingana na uwezo wake, unapompa masomo mengi unamfanya asiweze kuelewa haraka kwa kuwa bado akili yake inahitaji kukomaa ili aweze kupewa majukumu hayo.
“ Utekelezaji wa (BRN) ni mgumu sana kulingana  na mfumo wa elimu ulivyo mazingira na baadhi ya mabadiliko ya mfumo unafanya pawe na ugumu wa watoto kufanya vizuri japo kuwa tunajitahidi sana katika kuwafundisha ila masomo saba kwa mtoto wa darasa la kwanza   bado ni tatizo ,
“Utakuta mtoto wa darasa la kwanza ana begi kubwa limejaa madaftari na vitabu mpaka utamwonea uruma anavyo elemewa na hilo begi nabado anafika mpaka darasa la tatu hajui kusoma kwa ufasaha”anasema Muhimbula
Anasema japokuwa masomo hayo yameongezwa lakini bado kuna tatizo la walimu katika baadhi ya masomo uku tukihitajika kualika wageni waje kufundisha somo husika kwa kuwa limekosa mwalimu wa somo.
“Kuna kompyuta tatu shule nzima ambayo inawanafunzi wapatao 2000 na izo kompyuta wazazi ndio wamechangia kuleta na bado kunatatizo la walimu inafikia kipindi inabidi tuwalike wageni kwa kweli bado kunasari ndefu sana katika kutekeleza matokeo makubwa sasa(BRN)”anasema Muhumbula
Mwalim anasema wazazi wanapaswa kuwafatilia watoto wao katika maendeleo ya Elimu na kuakikisha wanafanya vizuri kwa kuwa mazingira yamebadilika sana,mitando ya kijamii,simu za mkononi na mfumo wa maisha umebadilika sana sio kama zamani unahitaji mzazi awe makini kumlinda mtoto.
“Nikweli kuna baadhi ya watoto sio wasikivu wanacho ambiwa na wazazi lakini suala la kutoa elimu lisiwe kwa mwalimu bali kila mmoja tuwajibike katika kutoa Elimu ili kuwasaidia hawa watoto.
 “Pia wazazi wasikate tamaa kutokana mazingira ya sasa ni hatari sana kwa malezi ya mtoto,wanapaswa kuwakumbusha wajibu wao mara kwa mara bila ya kuchoka ili kumfanya mtoto akue kwenye madili mazuri”anasema Muhumbula
Naye Mwalim Mkuu Msaidizi Christina Wambura anaongeza kusema mlundikano wa wanafunzi katika darasa moja unampa shida mwalim katika kutimiza majukumu ya kuakikisha kila mwanafunzi anaelewa anachofundishwa.
“ Utakuta darasa lina wanafunzi 60 mpaka 70 badala ya 45 idadi inayotakiwa,kwetu imechangiwa na kuwepo kwa shule moja ndani ya kata yetu ambapo utakuta wanafunzi wengi wanatoka mbali kama vile gongo la mboto,kigamboni na pugu na kusababisha kupokea wanafunzi wengi tafauti na idadi”anasema
Anasema bado kuna tatizo kwenye upande wa masomo kama Tehama ambalo linahitaji kuwa na walimu wenye ufahamu wa somo hilo linalo hitaji kujua Technolojia.
“Bado somo la Tehama linatoa changamoto kubwa kwa kuwa hakuna walimu wenye ujuzi inafika wakati inatubidi kuarika mgeni ili wanafunzi wasome”anasema Wambura










No comments:

Post a Comment