Tuesday, 15 July 2014

Bado Israel inaendelea kukiuka sheria za kimataifa




Pendekezo la kuweka chini silaha lililotolewa na Misri na kukubaliwa na Israel haliheshimiwi.Jeshi la Israel limeanza upya kuhujumu vituo vya wapalastina huko Gaza kufuatia kuendelea kufyetuliwa makombora ya Hamas dhidi ya Israel.Muda mfupi kabla ya hapo baraza la usalama la Israel liliunga mkono pendekezo hilo.Tawi la kijeshi la Hamas limelipinga pendekezo hilo lakini afisa mmoja wa tawi la kisiasa alisema tunanukuu:"Hakuna aliyezungumza na sisi.Pendekezo tumelisikia kupitia vyombo vya habari.Tunashukuru kwa juhudi zinazofanywa.Lakini tunataka kuzungumza ana kwa ana na Misri.Tukae na kushauriana na baadae tutatoa jibu letu kwa pendekezo hilo na marekebisho ya aina gani tunayahitaji."
Waziri mkuu wa Israel alisema hapo awali makombora ya Hamas yakiendelea kufyatuliwa dhidi ya Israel,basi hujuma za madage ya kivita ya nchi yake zitazidi makali.Matamshi hayo aliyatoa Netanyahu wakati wa mkutano na waandishi habari pamoja na waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier

No comments:

Post a Comment