Monday, 14 July 2014

Ukatitili wa kijinsia bado unawamaliza wakina mama wengi



MATUKIO ya ukatili wa kijinsia ni moja ya mambo yanayorudisha nyuma harakati za kumkomboa mtoto wa kike katika ukatili wa kijinsia.
Zipo njia nyingi zinazotumika kuendesha matukio ya ukatili wa kijnsia ikiwemo ajira za majumbani, ambazo kwa asilimia kubwa zinaendelea kuchochea suala hilo huku walengwa wakiwa hawajui sehemu ya kwenda haki zao.
Baadhi ya watu katika jamii ambao wamekuwa si waaminifu wamekuwa wakiitumia dhana ya ajira za majumbani kuendesha vitendo vya kijinsia.
Watu hao mara nyingi katika kutekeleza uovu wao wamekuwa wakienda vijijini na kuchukua wasichana wadogo kwa kuwarubuni kuwaleta Dar esSalaam kwa ajili ya kufanya kazi za ndani huku wakijua si kweli.
“Katika mradi wetu tulibaini kuwa wapo watu ambao wanakwenda vijijini wanachukua wasichana na kuwaahidi kuwa wanawaleta kwa ajili ya kazi za ndani, lakini baadaye inakuwa tofauti, kuna mfano mmoja ambao tumeuona Bagamoyo ambako tunaendesha mradi huu pia, msichana alichukuliwa kutoka Ludewa kuwa analetwa Dar es Salaam kwa ajili ya kazi za ndani, lakini baadaye kumbe huyo mtu alikuwa na lengo jingine kichwani mwake.
“Mtu huyo aliyejifanya ni msamaria mwema kumbe lengo lake alitaka kuishi naye kama mke na mume, binti yule mdogo mwenye umri wa miaka 16 hakukubali kitendo, siku moja waelimishaji rika ambao tuliwapa mafunzo maalum walipata taarifa juu ya jambo lile na walikwenda hadi katika nyumba ya yule mhusika aliyejifanya msamaria mwema na kumchukua kwa ajili ya kumpatia msaada,” anasema Dk. Makula.
Anasema baada ya kuhojiwa msichana huyo alieleza jinsi alivyochukuliwa na ahadi aliyopewa lakini alijikuta Bagamoyo akitakiwa kuwa mke jambo ambalo hakukubaliana nalo.
 “baada ya kupata maelezo yake walimsaidia lakini pia walimpeleka  kituo cha polisi na kufungua jalada na baada ya taarifa zile kumfikia mhusika alikimbia lakini hadi sasa hivi anatafutwa kwa ajili ya kuchukulia hatua za kisheria,” anasema Dk Makula.
Anasema kupitia mradi wao wa kupinga ukatili wa kijinsia na mapambano ya Maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (GBV/HIV ambao unafanyika katika kata kumi na sita Wilayani Bagamoyo wameweza kufanikiwa kufanya kazi kwa ukaribu na wanajamii ambako wameweza kuibua matukio makubwa.
Dk.Makula anasema baada ya kuwapata wasichana waliokumbana na masuala ya ukatili wa kijinsia huanza kuwahoji, kufikisha mashauri yao kwa wenyeviti wa serikali za mitaa na baadaye Polisi kwa ajili ya kufungua mashitaka.
“Hawa wana mawasiliano jamii tumewapa elimu ya kutosha kuweza kupata taarifa sahihi kwa kila mtu wanayesikia amepata matatizo ya ukatili au masuala ya Ukimwi, tunazungumza nao kwanza wajue njia gani watanatakiwa kuzipitia kuweza kupata haki zao, pili tunawaelekeza namna ya kufuatia kupata hizo haki na sisi wenyewe tukiwasaidia,tunaendesha programu hii kwa msaada wa Mfuko wa dharura wa Kimataifa wa kusaidia mapambano dhidi ya Ukimwi ( RFE).
Anasema wameweza kutoa mafunzo kwa wanamawasiliano jamii ambao kwa elimu waliyopata wameweza kuleta mabadiliko katika jamii wanayoishi.
“Kumekuwa na mwamko kwamba watu wanaweza kutoa taarifa za matatizo wanayokumbana nayo katika jamii,sasa hivi wanawake au wasichana wakifanyiwa masuala ya ukatili wa kijinsia wanakuwa tayari kutoa taarifa tofauti na mwanzoni, mwako umekuwa mkubwa tofauti na mwanzoni,” anasema Dk.Makula.
Anasema baadhio ya watu katika jamii wamekuwa si wa kweli kwani wamekuwa wakiwachukua wasichana vijijini kwa ahadi za kuwapatia kazi za ndani kitu ambacho si kweli.
“Sasa hivi baada ya elimu kuwafikia vizuri imekuwa rahisi, kwasababu hawa wasichana wanaofanyia ukatili kwa dhana kwamba wanakuja kutafutiwa kazi za ndani ni wengi, jamii imekuwa ikibadilisha mbinu kila wakati, lakini sasa hali inaanza kuabdilika kwamba inapotokea mtu anakumbana na jambo lile basi wanakwenda kutoa taarifa.
Suala la ukatili wa kijinsia limekuwa likikuwa kila siku kutokana na kadri jamii inavyobadilisha mfumo wa maisha.
Imekuwa kawaida kwa watu kutumia vigezo vya kutafuta wafanyakazi wa ndani lakini baadaye wengi hutelekeza katiia maeneo mbalimbali baadaya kufanyiwa ukatili wa kijinsia ikiwemo kubakwa na wakati mwingine kuambukizwa Virusi Vya Ukimwi.
Jamii kwa kushirikiana na serikali imekuwa ikipigia kelele suala hili lakini mara nyingi wasichana hao ambao ni wahusika wakuu wamekuwa hawana taarifa sahihi za wapi waende kutoa taarifa kwa ajili ya kupata msaada wa kisheria.

Mwisho





No comments:

Post a Comment