Saturday, 19 July 2014

Badili Mangula:Hawataka VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) kuwacha kufanya kazi kwa mazoea



 Kada wa CCM, Badili Mangula akitoa mada
VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)wametakiwa kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wafuate katiba ili waweze kuwa na moyo wa kizalendo na uwajibikaji.
Hata hivyo viongozi hao wanatakiwa lazima wawe wametosheka na wasitawaliwe na tamaa jambo ambalo litawawezesha kufanya kazi kwa ufasaha zaidi na kufikia malengo.
Hayo yalisemwa jana na Katibu wa CCM wa jimbo la Kawe, Badili Mangula alipokuwa akitoa mada ya wajibu na majukumu ya katibu kwa mujibu wa katiba ya Chama katika semina ya kuwajengea uwezo watendaji na viongozi wa Chama na jumuia wa ngazi ya kata katika jimbo la Temeke.
“ wakati umefika kwa viongozi kupewa semina lengo likiwa ni kuwajengea uwezo na kuwaongezea uelewa ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi”alisema Mangula.
Naye mwenyekiti wa CCM wa wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge ambaye alitoa mada iliyohusu wajibu na majukumu ya mwenyekiti wa CCM kwa mujibu wa katiba alisema mafunzo ni muhimu kwa kuwa yameelekezwa ndani ya katiba.
“Mafunzo si utashi wa mtu bali yamo ndani ya katiba ya chama hivyo ni lazima yatolewe kwa viongozu hao ili wawe na  weledi wa kufanya kazi ambao utakifanya Chama kiendelee kushika dola,” alisema.
Kwa upande wake mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu aliwataka viongozi hao wanaopata mafunzo hayo kuhakikisha wanaenda kuyafundisha kwa viongozi wa matawi ili nao waweze kuongezewa uelewa.
Alisema semina hiyo ni muhimu kwa viongozi hao kwa sababu inasaidia kuwapatia mbinu mbadala zitakazowasaidia katika kukipatia chama ushindi kwenye chaguzi zijazo.
@@@


No comments:

Post a Comment