Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeidhinisha ruhusa kuingia kwa misaada ya kiutu katika maeneo ya waasi bila ya ridhaa ya serikali ya Syria katika maeneo manne ya vivuko mpakani na Uturuki, Iraq na Jordan.
Hata hivyo Syria imetoa onyo kwa baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa inaiangalia hatua hiyo ya kupeleka misaada kuwa ni kuingilia ndani ya mipaka yake.
![]() |
| Baraza la Usalama likipiga kura kuhusu azimio kuhusu Syria |
Azimio hilo ambalo lilipitishwa kwa kauli moja litakalodumu kwa muda wa siku 180 na mfumo wa uchunguzi kwa ajili ya upakiaji wa shehena ya misaada katika milolongo ya magari katika nchi jirani, ambazo zitaiarifu tu Syria kuhusu aina ya msaada huo wa kiutu katika shehena hizo.
Watu milioni kadha wanahitaji msaada
Umoja wa mataifa umesema kuwa kiasi ya watu milioni 10.8 nchini Syria wanahitaji msaada, ambapo watu milioni 4.7 wako katika maeneo ambayo ni vigumu kufikiwa.
Kiasi ya watu 150,000 wameuwawa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria , ambavyo viko katika mwaka wa nne hivi sasa.
Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Samantha Power ameishutumu serikali ya Syria kwa kutumia kuzuwia misaada , kama "silaha nyingine katika hazina ya silaha zake za maangamizi na za kikatili dhidi ya maeneo yanayoshikiliwa na upinzani."
![]() |
| Majeshi ya serikali yakipambana na waasi nchini Syria |
Balozi wa Syria katika Umoja wa Mataifa Bashar Ja'afari ameliambia baraza hilo baada ya kura iliyopigwa jana kuwa serikali ya Syria inategemea jukumu lisilo elemea upande wowote, linalotekelezeka na la uwajibiukaji kutoka kwa Umoja wa Mataifa katika kushughulikia hali ya kiutu nchini Syria, hususan inapokuja suala la kuheshimu mipaka ya Syria.
Azimio hilo pia linaidhinisha upelekaji wa misaada kuvuka mipaka ya maeneo yenye mzozo.
Bashar al-Assad kuapishwa Alhamis
Wakati huo huo rais Bashar al-Assad katika sherehe za kuapishwa siku ya Alhamis anatarajia kujiweka katika hali ya kuwa "mshindi " wakati akijaribu kuwavutia Wasyria ambao wamechoshwa na vita pamoja na wale ambao wanahofia kusonga mbele kwa makundi ya kijihadi.
![]() |
| Kiongozi wa kundi la Taifa la Kiislamu Abu Bakr al-Baghdadi |





No comments:
Post a Comment