
Afisa mmoja anayesimamia oparesheni za misaada ya Umoja wa Mataifa Robert Turner amesema kuwa idadi ya wanaotoroka ni kubwa mno na ilivyotarajiwa na kwamba wakimbizi wapya watalazimika kulala katika sakafu.
Takriban raia mia tatu na hamsini wa Kipalestina wanadaiwa kuuawa tangu Israel ianzishe mashambulizi yake katika eneo la Gaza,ambalo inasema inajibu mashambulizi ya roketi yanayotekelezwa na wapiganaji wa Hamas.
Hapo jana Israel imesema kuwa wanajeshi wake wawili waliuawa baada ya wapiganaji kuingia Israel kupitia handaki moja.
No comments:
Post a Comment