Thursday, 17 July 2014

Mpango wa kusitisha mapigano waelekea kukwamishwa na pande zote


Makombora matatu yaliyofyatuliwa kutoka Ukanda wa Gaza yamepiga kusini mwa Israel, ikiwa ni saa mbili tu baada ya makubaliano ya kusitisha mashambulizi kuanza kutekelezwa. Jeshi la Israel limesema makombora hayo yalianguka katika eneo la Eshkol, ambalo liko katika mpaka wa Kusini mwa Ukanda wa Gaza. Hamas imekanusha kuhusika kwa vyovyote na shambulizi hilo. Ihab Ghusein, mkuu wa habari wa serikali ya zamani ya Hamas katika Ukanda wa Gaza, imesema makubaliano ya kuweka chini silaha yalikiukwa na Israel ambayo ilitumia vifaru kufanya mashambulizi wakati wa kipindi hicho. Jeshi la Israel baadaye lilisema mlipuko karibu na mpaka ulimjeruhi mwanajeshi mmoja, bila kutoa maelezo zaidi. Jeshi lilijibu kwa kufyatua makombora. Mashambulizi hayo yalivuruga mpango wa kuweka chini silaha uliosimamiwa na Umoja wa Mataifa kwa misingi ya kibinaadamu, ambao Israel na Hamas walikubali kuutekeleza kwa muda wa saa tano hapo jana.

No comments:

Post a Comment