Thursday, 31 July 2014

Taarifa za usajili:Arturo Vidal kutua Man Utd,Khedira kwenda Arsenal huku Chelsea mbioni kutoa offer kwa Aubameyang.



 muda mfupi hujao Arturo Vidal anatarajiwa kuongea na klabu yake Juventus juu ya kubadili uwamuzi wake na kuweka wazi mpango wake wa kujiunga na Man Utd baada ya tetesi za muda mrefu.

Juventus inajitaidi kupambana kwa hali yeyote kuakikisha mchezaji huyo mwenye asili ya Chilean anabakia katika klabu hiyo lakini wakala wake anaonekana kukubaliana na Man Utd..
Arsenal wakiwa tayari wameshasajili wachezaji wapatao wanne huku wakitalajia muda mfupi kupata huduma ya kiungo mkabaji wa Real Madrid Sami Khedira kutua Emarates.

 Madrid wapo tayari kumuuza  Khedira kuliko kumuacha klabuni hapo huku mkataba wake ukiwa umebakia mwaka mmoja kumalizika.

Edinson Cavani amekili kwamba kuna uwezekano wa yeye kujiunga na Man Utd ili kufanya uwezekano wa Angel Di Maria kutua katika klabu hiyo ya PSG.


Hata hivyo,striker huyo wa Uruguayan amedai kuwa bado anaitaji kubakia  Paris Saint-Germain msimu hujao.

Huku ikidaiwa kwamba Pierre-Emerick Aubameyang amekataa kupokea offer kutoka kwa Chelsea katika kipindi hiki cha usajili.

Tetesi hizo zinakuja baada ya The Blues kuwa na mpango wa kuuza vifaa vyake ikiwa ni pamoja na  Romelu Lukaku, Demba Ba na Samuel Eto'o kipindi iki cha usajili.

Upinzani kumburuza Obama mahakani

Baraza la Wawakilishi la bunge la Marekani linaloongozwa na chama cha Republican lapiga kura Jumatano (30.07.2014) kumshtaki Rais Barack Obama kwa madai ya kukiuka madaraka yake ya kikatiba.
Baraza hilo limepiga kura 225 dhidi ya 201 kuunga mkono hatua hiyo isio na kifani ya kumburuza rais mahakamani kwa kutotii sheria ipasavyo wakati akiutekeleza muswada wake wa marekebisho ya huduma za afya unaojulikana kama "Obamacare"
Hatua hiyo itamwezesha spika wa baraza hilo la wawakilishi la bunge la Marekani John Boehner kuanza kushughulikia taratibu za kisheria za kumdhibiti rais ambaye amesema amelewa madaraka.
Boehner amesema suala hilo halihusu mvutano kuhusu wabunge wa chama tawala cha Demokrat au Republican bali ni suala la kutetea katiba na kuchukuwa hatua madhubuti wakati katiba hiyo inapohatarishwa.
Kutetea katiba
John Boehner Spika wa Baraza la Wawakilishi la Bunge la Marekani.
Amekaririwa akisema "Mko tayari kumuachia rais yoyote yule kuchaguwa sheria gani za kuzitekeleza na sheria gani za kuzibadilisha ? Mko tayari kumuachia yoyote yule kukivunjilia mbali kile kilichojengwa na waasisi wetu ? Msifikirie tu juu ya kiapo mlichokula bali fikirieni jinsi mlivyokula kiapo hicho mkiwa kama chombo kilichosimama pamoja.Hicho ni kitu pekee ninachowaomba leo hii kuitetea katiba kwa niaba ya wananchi tunaowatumikia."
Boehner amewaambia wabunge wenzake kwamba Obama amekiuka katiba mama ya nchi hiyo kwa kutofuata kikamilifu tafsiri ya kisheria wakati wa kutekeleza marekebisho ya sheria ya afya.
Kwa upande wake Rais Obama amepuuzilia mbali kwa kuikejeli hatua hiyo ya kutaka kumfungulia mashtaka wakati akizungumza kwenye hotuba aliyoitowa huko Kansas City katika jimbo la Missourri.
Amesema huku akishangiliwa na umma uliokuwa ukimsikiliza na kwamba "Badala ya kunishtaki kwa kufanya kazi yangu vizuri, nalitaka bunge kufanya kazi yake kuboresha zaidi maisha ya Wamarekani ambao ndio waliowapeleka bungeni."
Obama pia amewakumbusha wananchi kwamba kwa vyoyote itakavyokuwa ni wao ndio wataobebeshwa gharama za kulipia kesi hiyo mahakamani.
Demokrat yalaani hatua hiyo
Wabunge wa chama cha Demokrat nao hawakupoteza wakati kuilani kura hiyo ya kumfungulia mashtaka rais.
Mbunge mwandamizi wa Demokrat Nancy Pelosi naye ameghadhibishwa na hatua hiyo ya kwanza ya kumshtaki rais katika historia ya Marekani na kumlinganisha na mtu dalimu.
Nancy Pelosi kiongozi wa wabunge wa Demokrat katika Baraza la Wawaklishi la bunge la Marekani.
Amesema inatia kichefu chefu, ni siasa chafu na kutomheshimu kabisa rais.
Debbie Wasermann Schultz mbunge wa chama hicho kwa jimbo la Florida amesema ni jambo lisilo na tafakuri kwamba wabunge wa Republican baada ya kukosa cha kufanya hatimae wameamuwa kufanya kitu kumshtaki rais kwa kufanya kazi yake wakati wakigoma kufanya yao.
Ameongeza kusema laiti angeliweza kusema hiyo ni siasa chafu kuwahi kuishuhudia na amewataka wapinzani na wabunge wa Republican wasipoteze fedha za walipa kodi kwa azimio hilo na badala yake waungane na wenzao wa Demokrat kushughulikia changamoto nzito zinazoikabili nchi yao.

Watu 200 kufunikwa na mapolomoko ya udongo,India

Zaidi ya watu 200 wanahofiwa kukwama katika maporomoko ya udongo nchini India,huku 20 wakithibitishwa kufariki dunia katika kijiji cha kijiji cha Malin karibu na mji wa Pune lilikotokea janga hilo.
Kazi ya uokoaji inaendelea katika eneo hilo huku hali ya hewa mbaya ikidaiwa kuchelewesha harakati hizo.
Vikosi vya uokoaji vimeendelea na kazi ya kuwanusuru waliofukiwa na maporomoko ya udogo huo, japo kuwa mazingira magumu na hali mbaya ya hewa vinakwamisha shughuli hiyo.Maporomoko hayo yaliyokikumba kijiji cha Malin India karibu na jimbo la Maharashtra yamesababisha nyumba nyingi kusombwa huku watu wakihofiwa kunaswa pia katika eneo hilo.
Taarifa iliyotolewa na mwandishi aliyoko  katika eneo la tukio inasema jengo pekee linaloonekana kunusurika na janga hilo ni ya shule pekee, huku maeneo mengine yakiwa tambarale kabisa.
Narendra Modi ni waziri mkuu wa India na hapa anaelezea hatua wanazozichukua.
Maporomoko ya ardhi ni jambo la kawaida kutokea nchini India hasa kipindi cha mvua zitokanazo na pepo za Monsoon ambazo hunyesha kuanzia mwezi june hadi septemba kila mwaka.


Rais Ernest Koroma wa Sierra Leone atangaza hali ya tahadhari

Rais wa Sierra Leone ametangaza hali ya tahadhari kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Rais Ernest Bai Koroma ametoa agizo maeneo yaliyokuwa yakwanza kuripoti ugonjwa huo yadhibitiwe ipasavyo na kutengwa .
Rais Koroma aliagiza watu wasiruhusiwe kuingia au kutoka kwenye maeneo hayo chimbuko la mlipuko wa ugonjwa wa Ebola.
Maafisa wa Usalama ndio waliopewa jukumu la kutekeleza maagizo hayo kwa ushirikiano na maafisa wa Afya ya umma.
Kulingana na takwimu Ebola huua asilimia 90% ya watu walioambukizwa homa hiyo ambayo huchukua kuanzia siku 2-20 kujulikana iwapo mtu ameambukizwa.
Rais wa Sierra Leone ametangaza hali ya tahadhari
Hadi kufikia sasa Ugonjwa huo umewaua zaidi ya watu 672 katika matifa matatu ya Afrika Magharibi yaani Liberia Sierra Leone na Guinea huku mtu mmoja akifariki nchini Nigeria.
Rais Koroma ametangaza kuwa hataenda Marekani kwa mkutano baina ya viongozi wa Afrika na rais Obama.

WEMA amtaja DIAMOND kuwa chanzo cha ugomvi na mama yake

Staa wa filamu Bongo, Wema Sepetu ametaja sababu zinazomfanya aingie katika mgogoro na mama yake mzazi, Miriam Sepetu kuwa ni suala la uchumba wake na Nasibu Abdul ‘Diamond’ ambao alikuwa akiupinga mara kwa mara.
Akiongea  na  mwandishi, Wema alisema kwa muda mrefu alikuwa akitofautiana kauli na mama yake katika suala zima la uhusiano wake na Diamond lakini anamshukuru Mungu amemuelewa na sasa kila kitu kinakwenda sawa.
Wema Sepetu akiwa na mama yake, Mariam Sepetu.
“Mama nilikuwa nikimsihi sana juu ya uchumba wangu na Diamond lakini sasa tumefikia hatua nzuri namshukuru Mungu amekubali, maana siku hizi nikionana naye ananiuliza vipi mwenzako mzima, anaendeleaje, wakati mwanzoni haikuwa hivyo,” alisema Wema huku akiahidi kumkutanisha Diamond na mama yake.

Zitto atoa ya moyoni kuhusu Umoja wa katiba ya wananchi(UKAWA)

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), kwa mara ya kwanza ameibuka na kupingana na harakati za Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).
 
Zitto amesema hana uhakika wala hauamini Ukawa kama utakuwa umoja endelevu hadi kufikia Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, kwa sababu si mara ya kwanza vyama vya upinzani kuungana na kugawanyika.
 
Mbali ya kutokuwa na imani na umoja huo, pia ameitaka Serikali kusitisha mchakato wa Katiba Mpya hadi uchaguzi mkuu utakapomalizika.
Alisema ni vema mchakato huo ukasitishwa kwa sasa, kwani inaonekana wajumbe wa Bunge hilo wanafuja fedha za umma.
 
Zitto alitoa kauli hiyo juzi, wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Power Breakfast kinachorushwa na kituo cha redio cha Clouds cha jijini Dar es Salaam.
 
Alisema Watanzania wanakabiliwa na changamoto nyingi na si Katiba pekee.
 
Alisema siku zote Watanzania wamekuwa wakipenda kuwa na upinzani imara ambao watu wanaweka tofauti zao pembeni na kuungana dhidi ya chama ambacho kinaongoza, lakini haoni kama Ukawa utaendelea hadi kufikia kipindi cha Uchaguzi Mkuu.

 
Alisema hatua ya kusimama kwenye ajenda moja ya Katiba haitausaidia umoja huo, kwani kipindi cha uchaguzi mkuu kinakuwa na ajenda nyingi.
 
Alisema wananchi watapenda kusikia masuala ya kushughulikia rushwa, matumizi ya rasilimali, maji, umeme, afya na barabara.
 
“Mambo haya ndiyo yatakayowafanya wananchi waamue namna gani watakabidhi dhamana ya uongozi, si suala la Katiba pekee,” alisema Zitto.
 
Alisema tusijitoe ufahamu kwa kudhani kwamba hii ndio mara ya kwanza kwa upinzani kuungana.
 
“Kulikuwa na Kamati ya Mabadiliko ya Katiba (KAMAKA) pia katika chaguzi za mwaka 1995, mwaka 2000 wapinzani waliungana vilevile, lakini kila inapokaribia uchaguzi wamekuwa hawaelewani kwa kuwa kila mtu anataka chama chake kipeperushe bendera.
 
“Lakini kama Ukawa wataweza kuweka ajenda yao mpaka mwisho itakuwa jambo jema kwa wananchi wenyewe. Kwa sababu nchini kwetu tatizo kubwa ni usimamizi na uwajibikaji, kama ajenda itachukua nafasi naamini hali haitakuwa mbaya, lakini bado siamini na sina uhakika kama umoja huu ni endelevu kwa namna ambavyo tunaona, ni umoja ambao unatokana na matakwa ya sasa ya Katiba, wameungana kwa sababu ya serikali tatu, lakini aina gani ya serikali bado hili linaweza kuwagawa,” alisema.
 
…  mchakato wa Katiba Mpya usitishwe
Akitolea ufafanuzi hoja yake ya kusitisha mchakato wa Katiba Mpya, Zitto alisema ni vyema serikali ikausitisha ili kunusuru fedha za umma zisiteketee.
 
Alisema fedha hizo zinastahili kutumika kununua madawa, kuendeleza miradi ya maji na kusomesha Watanzania, hivyo hakuna sababu fedha hizo kutumika kwa ajili ya kupiga porojo na kutukanana ndani ya Bunge.
 
“Nashauri tuahirishe mchakato huu mpaka baada ya uchaguzi mkuu mwaka kesho, ndipo hapo tuwe na mamlaka ya kujadili mchakato huu na kumaliza.
 
“Pia uchaguzi unaweza kuchekecha na ukaondoa baadhi ya watu ambao ni vikwazo katika mchakato kwa sababu uchaguzi hauna muamala, mtu ambaye alikuwa mbunge anaweza kuondolewa,” alisema.
 
Aidha, alisema kabla ya kwenda kwenye uchaguzi mkuu, Katiba ya sasa inatakiwa kurekebishwa baadhi ya maeneo ambayo ni vikwazo, kama vile Tume huru ya uchaguzi, kipengele cha wagombea binafsi kiwekwe na maeneo ambayo Zanzibar wamekuwa wakiyahitaji katika Katiba mpya, kwa mfano suala la mafuta na gesi yawekwe.
 
Alisema hakuna sababu ya kugawa nchi na kutumia rasilimali zilizopo kwa kufanya kazi ambayo haina matunda.
 
…amtetea January
Katika hatua nyingine, Zitto, ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, alisema amesikitishwa na mashambulizi yanayoelekezwa kwa Mbunge wa Bumbuli (CCM), Januari Makamba, baada ya kutangaza nia ya kuwani urais mwaka 2015.
 
Alisema kila kijana anapojitokeza kwa ajili ya kutaka kushiriki katika mamlaka za nchi, hasa katika nafasi kama hiyo ya urais, kumekuwa na mashambulizi makubwa dhidi yake.
 
Ni hatua ambayo sio nzuri kwa sababu kwa mujibu wa takwimu, idadi ya watu asilimia 72 wapo chini ya miaka 30, asilimia 65 ya wapiga kura ni vijana wenye umri kuanzia miaka 18 hadi 40, hivyo vijana wana haki ya kushiriki katika uongozi wa nchi, tufahamu changamoto za maendeleo ya nchi yetu zinahitaji uongozi mpya wa kizazi kipya.
 
“Ni dhahiri neno ujana si sifa, lakini neno uzee pia si sifa, hivyo tunatakiwa kuwapima vijana kwa sifa zilizopo, kama vile za kikatiba na zile za ziada, badala ya kusema vijana hawajakomaa… nilisikitika sana na mashambulizi ambayo yalielekezwa dhidi ya Makamba, natoa wito kwamba tuache, kwani wenye uamuzi wa mwisho ni wananchi.
 
“Mtu akigombea na kama akitoa sera zake vizuri wananchi wakamwelewa, akichaguliwa ni wananchi wameamua, hakuna mtu mwenye mamlaka kuwa fulani ni kijana, nadhani lazima tubadilishe uongozi na watu wajue nchi hii ni ya vijana, hatusemi wazee hawawezi ila wao wabaki kuwa washauri kama wao walivyokuwa vijana katika kipindi cha Nyerere nao walikuwa na miaka 40. Hivyo kuna haja ya kuweza kufikia hapo, changamoto za nchi ni kubwa, kuna haja ya aina mpya ya uongozi na mimi naamini aina hiyo itatoka kwa viongozi vijana,” alisema.
 
Hiyo ni mara ya kwanza kwa Zitto, ambaye yuko ndani ya Chadema kwa sababu za kisheria, kuibuka na kuuzungumzia Ukawa.
 
Mwanasiasa huyo kijana amekuwa kimya kwa muda mrefu, hata kwenye harakati za Ukawa amekuwa aghalabu kuonekana, hali ambayo imekuwa ikiibua maswali yuko upande gani katika mchakato huu wa Katiba Mpya.
 
Kauli hii ya Zitto inaweza kuibua fikra mpya kwa baadhi ya watu ambao wamekuwa na imani kubwa na umoja huo unaoviunganisha baadhi ya vyama vya siasa nchini.

Majina ya Wanaopiga Mabomu Arusha kuwekwa hadharani

Watuhumiwa wa mabomu katika maeneo mbalimbali mkoani Arusha, watawekwa hadharani hivi karibuni ikiwa ni pamoja na umma kuelezwa kilichotokea na waliowatuma.
 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisema hayo juzi alipokuwa akihutubia sherehe za Baraza la Idd jijini Dar es Salaam.
 
Alisema ingawa hatua za kisheria zinaendelea kwa baadhi ya watuhumiwa kufikishwa mahakamani na kufunguliwa kesi, serikali pia itaweka wazi juu ya matukio hayo ya mabomu, ikiwemo wanaowatuma.
 
Alisema kinachosubiriwa ni kukamatwa watuhumiwa wengine kama wawili, ambapo aliomba wananchi kushirikiana na Serikali  watiwe mbaroni.
 
“Serikali haikulala tangu tukio la kurushwa kwa bomu pale  Olasiti, tuliongeza nguvu ya wataalamu wa upelelezi kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na dalili nzuri zimeanza kuonekana.
 
“Napongeza vyombo vya ulinzi na usalama, tumekamata kundi kubwa na baadhi  yao wamekiri kushiriki mambo kadhaa na tutakuja kuwashirikisha,” alisema Pinda.
 
Alitaka jamii kufichua watu wote wenye  nia ovu ya uhalifu ili wananchi na jamii nzima iishi kwa amani. Alitaka viongozi wa dini kuepuka mifarakano ndani ya dini kwa kuwa inasababisha chuki zisizo na msingi.
 
Alisema mifarakano ndani ya dini ni mibaya na inapotoka nje na kuwa kati ya dini moja na dini nyingine, inakuwa mbaya zaidi na kuwasisitizia viongozi wa dini, kuhakikisha kila dini waumini wanakuwa na amani, utulivu na mshikamano.
 
Pinda alisema  anaamini amani na utulivu wa Tanzania, msingi wake ni mafundisho ya dini. Alisisitiza taifa lolote ambalo halina msingi huo wa dini, watu wake hawana tofauti na wanyama , kwa kuwa hawana hofu ya Mungu na hivyo hawaogopi lolote.
 
Alipongeza viongozi wa dini wa Dar es Salaam kwa kuunda Kamati ya Amani, inayohusisha viongozi wa dini za Kiislamu na Kikristo  ambayo hukutana na kujadili  namna ya kuboresha amani bila kujali tofauti zao.
 
Kutokana na ubunifu huo wa viongozi wa Dar es Salaam,  Pinda alisema kila mkoa anaokwenda, amekuwa akiwahamasisha wakuu wa mikoa kusaidia kuandaa kamati kama hizo kwa kuwa ni msingi wa amani.
 
Baraza la Waislamu wa Tanzania (Bakwata) wilayani   Arumeru,  limeahidi  kushirikiana na  polisi mkoani kuhakikisha linafichua watu ambao wamekuwa wakijihusisha na uvunjifu wa amani mkoani Arusha.
 
Kiongozi wa Baraza la Wazee, Wilaya ya Arumeru, Shehe Haruna Husein  alisema hayo jana akizungumza na waandishi wa habari kulaani vikali vitendo mbalimbali vya uhalifu vinavyoendelea mkoani humo.
 
Alisema, “Bakwata wilayani Arumeru inalaani vikali vitendo hivyo vya uhalifu vinavyoendelea mkoani hapa.” Alisisitiza watashirikiana na polisi kufichua wahilifu.
 
Alipongeza Polisi kwa jitihada zao kudhibiti uhalifu. Alitoa mwito kwa wahisani wengine kuhakikisha wanashirikiana na jeshi hilo kuwezesha wahalifu wakamatwe.
 
“Kwa kweli sisi kama Bakwata tunalaani vikali sana hivi vitendo vya uhalifu vinavyoendelea mkoani hapa, huku tukiahidi kushirikiana na jeshi la polisi katika kudhibiti matukio ya uhalifu yanayoendelea mkoani hapa ili wahalifu wote wanaojihusisha na matukio hayo wachukuliwe hatua kali za kisheria,” alisema.
 
Miongoni mwa matukio ya ulipuaji mabomu ni pamoja na kwenye Kanisa Katoliki, Parokia ya Joseph Mfanyakazi, Olasiti. Katika tukio hilo, watu wawili walipoteza maisha na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa.
 
Tukio lingine la ulipuaji bomu, ni kwenye mkutano wa wa Kampeni za uchaguzi mdogo wa Madiwani wa Chadema katika eneo la Soweto, ambalo pia watu kadhaa walipoteza maisha na wengine kujeruhiwa.
 
Hivi karibuni, mlipuko mwingine ulitokea katika mgahawa wa Vama Traditional Indian Cuisine na kusababisha majeruhi. Baadhi ya watu wanaodaiwa kuhusika katika ulipuaji wameshafikishwa mahakamani.
 
Tukio lingine la hivi karibuni ni la Katibu wa Bakwata, mkoani Arusha, AbdulKarim Jonjo aliyejeruhiwa na mgeni wake baada ya kurushiwa bomu nyumbani kwake, eneo la Esso wakati akipata daku na mgeni wake

Kingwendu kuchukua hatua baada ya mkewe KUBAKWA akiwa amelewa

Muigizaji wa filamu za Kiswahili, mchekeshaji Kingwendu yuko katika wakati mgumu baada ya mkewe kubakwa na jirani yake wakati akiwa amelewa pombe.
 
Baada  ya  jitihada  nyingi  za  kumtafuta Kingwendu, hatimaye  mwandishi  alifanikiwa  kumpata  na  kukiri  kuwa  alizipata habari hizo wakati ambapo yuko safarini na majirani walimueleza kilichotokea kuwa mkewe na jirani huyo aliyembaka mida ya saa tano usiku wote walikuwa wamelewa.
 
”Kama ulivyosikia hiyo habari, mimi nilikuwa sipo ndo nimerudi juzi, nataka nianze kufuatilia sheria sema sasa hivi nimefiwa na dada yangu tunapeleka msiba kijijini na baada ya hapo ninapumzika halafu ninasafiri Nairobi, nikirudi Nairobi tarehe tano kuanzia tarehe sita ndo naanza kufuatilia.” alisema Kingwendu.

Wednesday, 30 July 2014

Msanii Mwingine wa Bongo Anaswa China Kwa Tuhuma za Madawa ya Kulevya

HUKU modo maarufu Bongo, Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’, akisota jela nchini China kwa skendo ya kukamatwa na madawa ya kulevya (unga), mrembo mwingine ambaye aliwahi kujaribu kuchomoka kisanii kwenye muziki wa Kizazi Kipya almaarufu kwa jina la Winnie Mandela, naye amenaswa na polisi nchini humo…Inasemakana alikuwa Amebeba madawa tumboni na kupita vizuizi vyote mpaka alipoingia mtaani ndipo msako wa Polisi ulipomkumba na kumtia nguvuni….Hali Imekuwa Mbaya sana China kwa Watanzania kwani wanaishi kama Sungura.


LOWASA akana kukifadhili chama kipya cha Siasa Nchini cha ACT-


Katika gazeti la Tanzania Daima toleo na.3536 la tarehe 30 Julai, kuna habari inayosema Lowassa aibukia ACT na kumuhusisha na Mbunge wa Kigoma Kaskazini(CHADEMA) Zitto Kabwe katika kile gazeti hilo kilichodai mikakati ya siri dhidi ya Chadema.
Habari hizo ni uzushi, na ni muendelezo wa mikakati ya kumchafua na kumgonganisha Mh Lowassa na wanasiasa wenzake wa kada na maeneo mbalimbali.Mh Lowassa kama walivyo wabunge wengine wa CCM amekuwa na uhusiano na wabunge wenzake bila kujali tofauti ya vyama vyao.
Mh Lowassa ni kiongozi makini ambaye hawezi kupoteza muda wake kujiingiza katika masuala yasiyo na tija kwa nchi, wananchi na ustawi wa demokrasia makini na endelevu nchini.Muda wake anautumia kusimamia utekelezwaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM jimboni kwake Monduli. “Mimi na chama chetu, tuko busy kutekeleza ilani yetu,kuwaletea maendeleo wananchi ili wazidi kutupa ridhaa ya kuwaongoza katika chaguzi zijazo” alisema Mh Lowassa. 
Hata hivyo,Mh Lowassa anathamini mchango wa vyama vyote vya siasa nchini pamoja na Chadema katika kujenga demokrasia yenye tija kwa taifa.

Baada ya kumwagana na Ciara, sasa Future kutoka na mrembo mwingine

Kwenye ishu ya mahusiano msanii wa Hiphop Future ana sifa ya kuwa na watoto wanne hivi sasa na wote wana mama tofauti. Kabla na uhusiano na Ciara alikuwa tayari na watoto watatu lakini wote aliwaacha na hivi sasa inasemekana imefika zamu ya Ciara.
Tetesi zinasema kwamba Future alikuwa ameachana na Ciara hata kabla ya kujifungua mtoto na hivi sasa anaonekana kuwa karibu sana kimapenzi na mbunifu wake wa mavazi anaitwa Tyrina Lee.
Future ameonekana akiwa na mwanamke huyo kila sehemu akiwa kwenye tour, sehemu za mapumziko hadi maisha ya huyo mwanamke yamebadilika akifanya shopping za gharama na vyanzo vinasema ni pesa za Future.
Tangu Ciara ajifungue mtoto, Future anatumia muda mdogo sana kwenda kumuangalia mwanae lakini muda mwingi wanatumia kuwa na Tyrina Lee. Ukitembelea ukurasa wa mwanamke huyo kwenye instagram kuna picha nyingi akiwa na Future ndani ya hotel au kwenye ndege ya tour.

Taarifa ya Jeshi la Polisi kuhusu ajali iliyotokea asubuhi ya leo Dodoma.




July 30 imesambaa Taarifa ya ajali ambayo imetokea mapema leo na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma ajali iliyosababisha vifo vya watu 17 kati yao wanaume 12, wanawake 5 na majeruhi kwa mujibu wa jeshi la Polisi Dodoma




 Ajali hiyo imetokea majira ya saa 08:00 asubuhi eneo la Pandambili barabara ya Dodoma –Morogoro ambayo imehusisha basi la kampuni ya Moro Best yenye namba T258 AHV ambalo lilikuwa likitokea Mpwapwa kuelekea Dar es Salaam.


Basi hilo lilikuwa likiendeshwa na SAID S/O LUSOGO liligongana na Lori namba T820CKU / T390CKT lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Dodoma likiendeshwa na GILBERT S/O ISAYA NEMANYA.
Taarifa ya kamanda wa Polisi inseam katika ajali hiyo watu 17 wamepoteza maisha kati yao wanaume ni 12 na wanawake ni 5. Pia watu 56 wamepata majeraha mbalimbali na wamelazwa katika Hospitali za wilaya ya Kongwa na Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma. Miongoni mwa waliofariki ni pamoja na dereva wa lori hilo pamoja na utingo wake.
Chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa lori kutokuwa na tahadhari kwa magari yaliyokuwa yanakuja mbele yake wakati anapita (overtake) gari lingine na kwenda kuligonga busi hilo.

MIDO atupiwa vilago ZAMALEK

MAISHA ya soka ya Mido yameingia ukurasa mwingine baada ya kufukuzwa kazi ya ukocha mkuu na klabu yake ya Zamalek jana jumanne.
Kocha huyo kijana mwenye miaka 31 aliripotiwa kuwa na mgogoro na bodi ya klabu na kusababisha kibarua chake kuota nyasi, japokuwa inasemekana kuwa ataendelea kuwa sehemu ya miamba hiyo kwa majukumu mengine.
Mido alirithi mikoba ya Helmy Toulan mwezi januari mwaka huu na aliiongoza timu hiyo kucheza mechi za mwisho za ligi ya ndani na kutwaa ubingwa wa kombe la Misri mbele ya klabu ya Smouha.
Licha ya kupata mafanikio hayo, Mido aliyekaa kwa miezi saba tu aliripotiwa kuwa na matatizo mengi na bodi ya klabu hiyo, lakini mshambuliaji huyo wa zamani wa Zamalek atapewa majukumu mengine klabuni hapo.

Yaya Toure sasa kuzeekea Man City

KIUNGO wa mabingwa wa England, Manchester City, Yaya Toure amesema anataka kubakia klabuni hapo kwa muda mrefu kadiri itakavyowezekana.
Nyota huyo mwenye miaka 31 mapema mwaka huu aliripotiwa kutimka Etihad baada ya wakala wake, Dimitri Seluk kusema kuwa Toure alijisikia kutothaminiwa na klabu baada ya kutotumiwa salamu za siku ya kuzaliwa mwezi mei.
Toure mwenye alieleza kuwa anavutiwa kujiunga na matajiri wa Ufaransa, Paris Saint-Germain.
Siku za nyuma Toure alisema kwamba, mashabiki wasisikilize maneno ambayo hayajatoka mdomoni mwake, lakini kila asemacho Dimitri ni sahihi kwasababu anazungumza kwa niaba yake, ingawa kwasasa anasisitiza kuwa wakati wote amekuwa kimya kuhusu furaha yake na hatima yake ya baadaye.

Obama atangaza vikwazo vya nguvu dhidi ya Urusi

Rais Barack Obama wa Marekani ametangaza kupanua uwigo wa vikwazo dhidi ya Urusi kufuatia mgogoro unaoendelea Ukraines.Tangazo hilo la Rais Obama linafuatia vikwazo vilivyotangazwa na Jumuiya ya Ulaya saa chache kabla ya hili la Marekani.
Vikwazo hivyo vilivyotangazwa Marekani imesema itaiwekea vikwazo Urusi katika maeneo ya nishati,silaha na uchumi.
Hata hivyo Rais Obama amekanusha madai kwamba vikwazo hivyo vyaweza kuanzisha vita baridi dhidi ya Urusi, bali amesema kuwa wanalenga kuhakikisha Ukraine inarejea katika hali yake na kufuatia machafuko yanayoendelea hivi sasa.

Ebola ni ugonjwa tishio Afrika Magharibi


Nchi ya Liberia imefunga mipaka yake iliyo mingi ya kuingia nchini humo ili kudhibiti kuenea kwa maambukizi mapya ya ugonjwa Ebola.
Hata hivyo katika kuongeza jitihada Zaidi nchi hiyo vituo vya uchunguzi vimewekwa katika baadhi ya mipaka ya kuingia nchini humo vikiwemo viwanja vya ndege.
Katika hatua nyingine moja ya shirikakubwa la ndege Nigeria la Arik Air limesitisha ndege zake kuelekea Liberia na Sierra Leone baada ya mtu mmoja kubaini kuwa na ugonjwa huo wakati akisafiri kwa ndege kuelekea Nigeria.
Hadi sasa virusi vya Ebola vimesababisha vifo kwa watu 660 Afrika Magharibi tangu ugonjwa huo ulipozuka mwezi February mwaka huu.
Nigeria pia inachukua tahadhali katika mipaka yake baada ya kuthibitisha kufariki kwa raia mmoja wa Liberia wakati akiwasili uwanja wa ndege wa Lagos.

Gari la Msanii DUDE lakamatwa kwa tuhuma za Ujambazi



GARI la muigizaji maarufu wa filamu Bongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ limekamatwa na Polisi jijini Dar es Salaam likihusishwa na tukio la ujambazi linalodaiwa kutokea Kijitonyama Mpakani usiku wa saa 5.15 Julai 21 mwaka huu.


Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika, gari hilo aina ya Vitz lenye namba za usajili T 360 BAJ, lilikutwa likiwa na vijana wawili ndani yake, waliotajwa kwa majina ya Seif Jafari na Longina Ramadhani, waliotaka kupora Bajaj yenye namba za usajili T 296 CSC iliyokuwa ikiendeshwa na Seleman Khalfani.


Inadawa kuwa muda mfupi baada ya kukamatwa, Dude alitokea Polisi na kulitambua gari lake, lakini maelezo yake hayakuwatosheleza Polisi hivyo kumshikilia katika kituo kidogo cha Polisi Mabatini hadi kesho yake alipodhaminiwa.

Tuesday, 29 July 2014

Kinu pekee cha umeme Gaza chashambuliwa

Israel imeendelea na mashambulizi yake dhidi ya Gaza, sasa ikilenga miundombinu, ambapo hivi leo kinu pekee ya kuzalishia umeme kimeshambuliwa sambamba na nyumba ya kiongozi wa Hamas, Ismael Haniya.
Naibu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Nishati ya Palestina, Fathi al-Sheikh Khalil, ameliambia shirika la habari la AFP kwamba kinu hicho cha umeme kimesita kufanya kazi kutokana na m
ashambulizi ya Israel usiku wajana, ambayo
yaliliharibu jenereta na matangi ya mafuta ambayo yaliripuka kabisa.
Mwandishi wa AFP ameshuhudia moto mkubwa karibu na kinu hicho asubuhi ya leo, akisema kwamba idara ya zimamoto hadi wakati huo ilikuwa haijaweza kulifikia eneo hilo.
Mashambulizi dhidi ya kinu hicho pekee yanaongezea madhila tu juu ya jaala ya Gaza ambayo kwa siku ya 22 sasa imekuwa ikitwangwa makombora ya Israel mfululizo. Kuharibiwa kwa kinu hicho kunamaanisha pia kwamba huduma ya umeme ambayo tangu hapo ilikuwa si ya uhakika, inazidi kuwa mbaya, kwani Gaza ilikuwa ikitumia kinu hicho pamoja na umeme inaonunua kutoka Israel, ambao nao sasa haupatikani kutokana na njia za umeme kuharibiwa vibaya na mashambulizi ya Israel.
Khalil amesema katika kila njia kumi za umeme ndani ya Ukanda wa Gaza, njia tano zimeharibiwa. Tayari hospitali, ambazo hata nazo hazisalimiki na makombora ya Israel, zimeanza kulalamikia uwezo mdogo wa nishati ya kuhifadhia maiti na kutibia majeruhi.
Nyumba ya Haniyeh yalengwa
Sehemu ya nyumba ya kiongozi wa Hamas, Ismail Haniyeh, iliyoshambuliwa na Israel usiku wa kuamkia tarehe 29 Julai 2014.
Usiku wa kuamkia leo pia umeshuhudia mashambulizi mengine dhidi ya makaazi ya raia, ambapo kombora lililorushwa kutoka ndege ya Israel liliangukia nyumba ya kiongozi wa Hamas, Ismail Haniyeh, ingawa kiongozi huyo na familia yake walinusurika kuuawa.
"Jana usiku wakati tumelala, milango ya saa saba unusu, maroketi yakaanza kuanguka, yalikuwa mashambulizi matatu tafauti. Tukawachukuwa watoto wetu wakiwa usingizini na kukimbilia upande wa kaskazini, lakini tunamshukuru Mungu hakuna madhara, hakuna majeruhi wala mashahidi, yote kwa rehema za Mungu kuwanusuru wapigania jihadi na Ismail Haniyeh," amesema jirani wa Ismael Haniye, Bi Fatima Abu Riyale.
Hamas pia inasema kuwa kituo chake televisheni na redio, vyote vinavyoitwa Al-Aqsa, pia vilishambuliwa, ingawa televisheni iliendelea na matangazo hata baada ya mashambulizi hao, huku redio ikizimika kabisa. Majengo mengine yaliyoharibiwa kabisa na mashambulizi ya hivi karibu ni kabisa ni Msikiti al-Amin na wizara ya fedha.
Kufikia leo, tayari Wapalestina 1,110 wameshauawa na zaidi ya 6, 500 kujeruhiwa, ambapo Umoja wa Mataifa unasema zaidi ya asilimia 75 kati yao ni raia. Israel imethibitisha kupoteza wanajeshi wake 53 na raia watatu, ingawa Hamas wanasema idadi ya wanajeshi wa Israel waliouawa ni wengi zaidi. Maelfu ya wakaazi wa Gaza wamegeuzwa kuwa wakimbizi wa ndani, ingawa hawana mahala pa kukimbilia palipo hasa salama.
Shinikizo la kimataifa linaongezeka kwa ajili ya kupatikana usitishwaji mapigano, ingawa Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ameapa kuendelea na mashambulizi hadi waiangamize kabisa Hamas.

Dudubaya atoa ya moyoni kuhusu Ugomvi wa Ali Kiba na Diamond............kwa habari zaidi ingia humu

Dudubaya anajulikana kama mmoja wa Wasanii wa siku nyingi bongoflevani ambae pamoja na headlines zake binafsi huwa anasikika mara chache akizungumzia au kutoa ushauri kwa ishu kadhaa za Wasanii wenzake. Baada ya kusikia yanayoendelea kati ya mastaa wa bongofleva Diamond na Ally Kiba kwamba wako kwenye beef, Dudubaya alikutana na AyoTV Dar es salaam na kuyasema yafuatayo >> ‘Wasanii wa Tanzania tuna wapambe na sio marafiki kwa sababu mpambe unaweza kuwa umelewa yeye ndio anakoleza ugomvi lakini rafiki ni yule anaekuonya au kukushauri’

Msanii DUDU BAYA

Ali Kiba alifanya ngoma na R.Kelly nikafurahia na nikapenda kinoma kupiga salute kwa mdogo wangu anakwenda next level, Diamond kaja kufanya vizuri na ninafurahia… muziki huu unakosa nguvu kwa sababu ya roho mbaya, wivu na chuki na kutokuwa makini na wanaotuzunguka, anakwenda kwa Diamond anasema hivi kisha anakwenda kwa Ally Kiba anasema hivi’ – Dudubaya ‘Ninachowashauri hawa wadogo zangu watulie chini wajitambue ni Wasanii na usanii wao ni wa kutengeneza pesa, tena watengeneze hata Tour ya Amani wazunguke nchi nzima.. wazunguke hata Afrika Mashariki na sio hizi beef’ ‘Siku moja nilikua na Dully Sykes na Christian Bella alafu watu wakawa wanasema Diamond ooohhh sijui kashindaje tuzo saba, nikawaambia hivi ukiwa na akili timamu wimbo kama ‘my number one’ kila kona unayopita, video mpaka TV za kimataifa zinapiga alafu leo unaweza video yako ya kijingajinga unategemea kuishinda ‘my number one’ …….Diamond alistahili kushinda hizo tuzo saba, mimi sikuona cha ajabu’ Kwenye sentensi nyingine Dudubaya amesema ‘kuna gazeti moja liliandika eti Diamond alihonga hela kuchukua hizo tuzo, ni vitu vya kipumbavu kabisa… hujui kusoma lakini picha lazima uione, Ali Kiba na Diamond kila mmoja ana mama yake, wakae chini kama binadamu wajitambue, waachane na mambo ya watoto wa hapa mjini hawa ni wapambe tu mwisho wa siku hawana msaada’ Unaweza kumsikiliza Dudubaya zaidi hapa kwa kubonyeza play kwenye rangi ya orange hapa chini.

Monday, 28 July 2014

HUWAKIKA:Arsenal wamemaliza usajili wa Calum Chambers muda mfupi uliopita

ARSENALimetangaza kusainiwa kwa mlinzi wa Southampton  Calum Chambers kwa ada thamani ya hadi £ 16m.
Chambers amekubali mkataba wa miaka mitano na inaaminika kuwa Arsene Wenger ana mpango
wa kuwavutia  vijana zaidi.
Wengeralisema: "Sisi tuna furaha  sana baada
ya kwamba Calum amekubali kujiunga nasi .
"Kwajinsi  alivyo onesha uwezo  Ligi Kuu msimu uliopita na Southampton katika umri mdogo inaonyesha kwamba yeye ana ubora mkubwa."Yeye ana mengi  kuangalia na kujifunza kwa kuwa bado  mchezaji kijana na nina uhakika kwamba atafanya vizuri zaidi akiwa hapa na sisi."alisema Wenger.
Chambers alisema: "Nina furaha kwa kusainiwa na Arsenal.
"Arsenal ni klabu nzuri  kwa aina yao ya uchezaji na timu ambayo ipo juu kwa miaka mingi.
"Mimi nina naangalia mbele ili kujiunga na  mfumo mpya wa timu wa apa  leo ​​ni mwanzo wa maandalizi ya msimu wa mbele.
"Napenda kuchukua fursa hii kusema asante kwa kila mmoja katika klabu ya Southampton FC kwa kila kitu walichonifanyia kwa ajili yangu na kwa ajili ya kufanya usajiri  uwezekane."
Mkurugenzi mtendaji wa Southampton Les Reed alisema: "tunapatwa na uzuni pale wahitimu wetu wa Academy wanapondoka klabu, na kuondoka kwa  Calum imetuumiza sana kuondoka kwake.
"Calum aliweka wazi kwetu kwamba hakuona siku za usoni  katika klabu Southampton.

"Msimamo wetu bado haujabadilika kwa kuwa sisi tuna nia ya kulea vijana wetu wawe bora wachezaji katika klabu bora, kama  inavyothibitishwa na uamuzi wa tuzo Harrison Reed mpya mkataba wa muda mrefu wiki iliyopita,na  kuongeza orodha ya wataalamu wa vijana nia kama James Kata Prowse, Sam Gallagher, Jack Stephens, Jordan Turnbull, Matt Targett, Sam McQueen na wengine ambao wameona mengi ya shughuli ya kwanza timu hivi karibuni.
"Ni muhimu katika uhamisho dirisha kubakia shwari, ushujaa  juu ya tulichokifanya ni uzuni wa klabu nzima.lakini bado klabu Tuna malengo."