
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana,Waziri
wa Nishati na Madini, professor Sospeter Muhongo alisema nafasi hizi
zinapatikana kwa ushindani baada ya kutangazwa kwenye vyombo vya habari.
Alisema
vigezo vinavyo tumika katika kupata
ufadhili ni aina ya kozi aliyoisoma
mwombaji katiaka shahada ya kwanza au uzamili,chuo alicho soma shahada
ya kwanza,kiwango cha ufaulu
katika shahada ya kwanza kuanzia GPA 3.0 na uwiano wa jinsia.
“Nafasi hizi
zinapatikana kwa ushindani baada ya kutangazwa kwenye vyombo vya habari ambapo
vigezo vinavyotumika kupata kupata ufadhili ni aina ya kozi uliyoisoma mwombaji,
”alisema muhongo.
Pia alisema
kuwa Serikali ya china imetoa ufadhili
wa nafasi kumi (10) za masomo kwa watanzania katika ngazi ya shahada
uzamili na uzamivu katika fani ya mafuta na gesi.
Alisema
katika shahada ya uzamili wamechaguliwa watanzania 9 kati ya 46 walioomba
ufadhili ambapo katika shahada ya
uzamivu amechaguliwa mtanzania mmoja kati ya wanne walio wasilisha maombi.
No comments:
Post a Comment