
Rai hiyo
ilitolewa jijini Dar es Salaam jana, wakati wa semina ya kutambua sifa za kiongozi
bora iliyowakutanisha zaidi ya wazee 100.
Mwakyembe
alisema, hakuna jambo lolote linaloweza kufanikiwa bila ya kushirikisha kauli
za wazee, hasa waliokuwa na busara katika utatuzi wa mambo mbalimbali ikiwemo
migogoro katika vyama.
“ Kauli ya
wazee ni dawa, lakini kutokana na kuwa nyuma kwenye suala la kujitolea
wanaonekana hawafai au wamepitwa na wakati, haya yote huenda yakatokana na
wengi wao kutotambua sifa zao katika jamii inayowazunguka”alisema.
Mwakyembe
aliwahakikishia wazee hao kuwa, Chadema itasimamia haki zao juu ya kuzitambua
sifa zao zitakazowasaidia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ili kuleta
mabadiliko yatakayowainua kiuchumi.
Hata hivyo,
aliwafafanulia baadhi ya sifa anazostahiki kuwa nazo kiongozi kuwa, awaze
mafanikio makubwa, awe na nia kwa jambo analotaka kuongoza, ajitambue mwenyewe,
asimamie maamuzi sahihi asiwe kigeugeu pia adhibiti msongo wa mawazo.
“Siku zote
uongozi ni dhima kuna wale wanaozaliwa na bahati hiyo huku wengine wakizisomea,
lakini yote sawa hivyo kiongozi bora
anatakiwa akubali kukosolewa, awe
msikilizaji na afuate haki, pia anatakiwa atie moyo watu pamoja na kufurahia
mafanikio”alisema.
Alisema, kuna
baadhi ya viongozi wamekuwa wasaliti kutoka na kutozingatia sifa za uongozi
ikiwemo kukubali lawama, kutoungana na watu wa chini yake, kushindwa kutatua
matatizo, kutojifunza kutokana na makosa pamoja na kukosa uaminifu.
Kwa upande
wake Mwenyekiti wa Wazee wilayani humo, Waziri Mkunguna aliwataka wazee wenzake
kuhakikisha wanajitolea katika mambo mbalimbali ya kukiendeleza chama hasa kwa
kuzingatia kanuni na sifa walizoambiwa.
MWISHOO.
No comments:
Post a Comment