WAANDISHI wa
habari wametakiwa kuacha kushirikiana na Taasisi binafsi na wanasiasa wasiokuwa
na nia njema ya kupatikana kwa katiba mpya.
Tahadhari
hiyo imetolewa na jana na Balozi wa Amani nchini, Risasi Mwaulanga aliyesema kuwa
wapo baadhi ya wanasiasa wenye nia ya kuwapotezea Watanzania fursa ya kupata
katiba mpya kwa maslahi yao binafsi.
Akitolea
mfano wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), alisema kwamba wamekuwa wakitumia
vyombo vya habari vibaya kwa nia ya kupoteza fursa ya Watanzania kupata Katiba
mpya.
Alitoa wito
kwa Ukawa kurejea bungeni kupambana kwa hoja na si kutumia propaganda za kupotosha
umma.
“Tangu
walipoanza Ukawa wamejipambanua kwa kuonyesha kwamba wapo tofauti na malengo ya
kupatikana kwa katiba huku kwa makusudi wamekuwa wakitumia vyombo vya habari
kufaanikisha malengo yao,”alisema Mwaulanga.
Alisema kuwa
kipindi kilichopita katika bunge maalumu la Katiba Mbowe alishawahi kusema
kwamba katiba mpya itapatikana kwa ngumi na mateke sasa cha kushangaza aanakuwa
mstari wa mbele kupinga upatikanaji wa katiba hiyo.
“Katika moja
ya vikao vya bunge la katiba awamu iliyopita, Mbowe aliwahi kusema kuwa, ni
lazima katiba ipatikane kwa ngumi au mateke. Lakini inashangaza leo kuwa mpingaji
naamba mojaa wa kupatikana kwa katiba mpya huku akiwa anatetea maslahi binafsi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment