Tuesday, 12 August 2014

Wassira kuwa mgeni rasmi katika maonesho ya tatu ya sayansi chipukizi



Waziri wanchi ofisi ya Rais sera na uratibu, Steven Wassira anatarajiwa kufunga maonesho ya tatu ya wanasayansi chipukizi katika ukumbi wa mwalimu Julius Nyerere.
 Pia Vijana wametakiwa kuwekeza katika suala zima la utafiti wa kisayansi ili kuleta maendeleo katika nchi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana,Kaimu mwenyekiti wa Sayansi chipukizi,Stephen Nyangonde alisema vijana wanafursa kubwa ya kujiinua kimaendeleo endapo watajikita kwenye masuala ya kisayansi.
“Kama vijana watajikita katika masuala ya sayansi watapata kujiinua kimaendeleo kwakuwa kuna fursa kubwa endapo watakuwa makini,”alisema Nyangonde.
Hata hivyo Nyangonde aliwataka vijana  kutumia taaluma ya sanaa ili kuhamasisha utafiti wa kisayansi .

No comments:

Post a Comment