Friday, 15 August 2014

Viongozi wa Serikali na waganga wa jadi wahusishwa na mahuaji ya viungo vya Albino yanayoendelea nchini



 CHAMA cha watu wenye ulemavu wa ngozi Tanzania (TAS),kwa kushirikiana na Taasisi za kutetea haki za binadamu pamoja na jumuia ya watu wenye ulemavu,na shirika la UNDER THE SAME SAME (USS) wameitaka Serikali kusitisha vibali vya waganga wa  jadi ili kukomesha suala zima la ukataji waviungo vya albino.
 Mbali na agizo hili pia wameitaka serikali kusitisha matangazo ya waganga wa jadi kwa madai kwamba wanapotesha jamii huku matukio ya ukatili yakiendelea.
Akizungumza na waandishi wa Habari jana jijini Dar es Salaam Meneja Uendeshaji wa TAS Gamariel Mboya alisema wamesikitishwa na kitendo cha kinyama alichofanyiwa mtoto wa miaka 15 Upendo Sengerema cha kukatwa Mkono wa kulia wiki iliyopita   katika kijiji cha Usinge mkoa wa Tabora.
Alisema tukio hilo ni la pili kutokea kwa kipindi cha miezi mitatu tangu kuanza kwa mwaka huu hali inayotishia amani ya kuishi kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.
“Kuendelea kukithiri kwa vitendo hivi vya kikatili  ni ishara tosha kuwa kama hatua za makusudi hazitachukuliwa uovu huu wa ukatwaji wa viungo utaendelea  huku walengwa wakubwa wakiwa ni waganga wa kienyeji pamoja na viongozi wan chi,”alisema Mboya.
Alisema imekuwa ni kawaida kila ifikapo kipindi cha uchaguzi matukio haya ya kikatili kuendelea kukua kwani ripoti ya uchunguzi inaonesha kuwa tangu mwaka 2006 mpaka sasa ni watu 73 waliouwawa ,watu 10 wamekatwa viungo, watu 46 walinusurika kukatwa na makaburi 18 yalifukuliwa.
Alisema mpaka sasa watu wenye ulemavu wa ngozi wamekuwa wakiishi kwa hofu kubwa jambo ambalo liawaathiri kisaikolojia na linarudisha nyuma maendeleo.
Alisema vitendo hivyo vya ukatwaji wa viungo unaonesha ni kwa kiasi gani serikali,wabunge pamoja na wanasiasa hwana nia ya dhati na utashi wa kisiasa ili kuweka mipango madhubuti na shirikishi ili kutathmini shughuli za waganga wa jadi.
   




No comments:

Post a Comment