Friday, 8 August 2014

BARAZA la habari (MCT) lapewa somo na Jaji kiongozi Mahakama kuu ya Tanzania



BARAZA la Habari Tanzania (MCT) limetakiwa kuendelea kusimamia uadilifu na kukuza weledi  wa tasnia ya habari nchini kwa kutokana na kutokuwepo kwa sheria yenye kuelekeza sifa mahususi za mtu anayestahili kuwa mwandishi wa habari.
Pia vyombo vya habari vimetakiwa kuweka utaratibu wa kutanguliza maslahi ya kitaifazaidi na si ubinafsi kwa sababu kwa sababu yanaweza kusababisha vurugu.
Hayo yalisemwa juzi na Jaji Kiongozi  Mahakama Kuu ya Tanzania, Shaban  Ally Lila alipokuwa alipokuwa anazindua bodi mpya ya MCT , alisema hata sheria ya magazeti haina kifungu kinachoweka bayana sifa ya mtu kuwa mwandishi wa habari hali ambayo inafanya kila mtu kujiona kuwa anaweza kufanya kazi hiyo, hivyo alishauri kuwe na vigezo vya mtu kuwa mwanahabari ili kudhibiti makanjanja.
“Heshima ya taaluma hii imekuwa ikichezewa, ni bodi tu ndiyo pekee ambayo inaweza kurekebisha na kudhibiti wanahabari uchwara, hivyo natarajia bodi hii mpya itatekeleza wajibu wake kwakiwango cha juu,” alisema.
Jaji kiongozi aliongeza kuwa maadili ya kazi ya uandishi wa habari huenda sambamba na umuhimu wa stadi za namna ya kutoa taarifa za kweli ambazo huweza kulikwamua taifa katika majanga mbalimbali, hivyo ni jukumu la vyombo hivyo kutanguliza  maslahi ya taifa na si ubinafsi.
Pia aliwashauri wahariri kukagua na kujiridhisha kwa taarifa mbalimbali kabla ya kutolewa katika vyombo vya habari  ambapo alitolea mfano katika habari za mahakama ni jukumu la wanahabari wakisimamiwa a MCT katika uandishi unaozingatia ufuatiliaji wa karibu wa mashauri yaliyo mahakamani kwa kuonana na viongozi kupata ufafanuzi wa kesi na kuzingatia nidhamu na kutoegemea upande wowote wa mwenendo.
Katika hatua nyingine kiongozi huyo alisema vyombo vya habari vimekuwa  mstari wa mbele katika kutoa maoni na kuelimisha umma kuhusu ubora na ubovu wa sheria zilizotungwa au zinazotarajiwa  kutungwa, ambapo vilisaidia sheria mbaya kuachwa kutumika au kurekebishwa pamoja na kutungwa sheria bora.
Hata hivyo alisema vyombo hivyo katika kutekeleza majukumu yake katika baadhi ya maeneo na matukio vimeingia kwenye tuhuma na lawama, ambapo alitolea mfano baadhi ya maeneo yanayolalamikiwa kuwa ni pamoja na kutoa habari zisizokuwa na ukweli, kuwa na mlengo mmoja, kudhalilisha na kukera, kutozingatia maadili na weledi.
 Pia alisema kuwa kuna malalamiko kuwa uhuru   vyombo vya habari  kuwa umeminywa na sheria ya magazeti  hasa katika kifungu cha 25 ambacho kinampa waziri anayehusikka kukifungia chombo cha habari ambacho kwa maoni yake kinakinzana na mila na maadili ya taifa, ila ni muhimu ikafahamika kuwa hakuna uhuru usiokuwa na mipaka.
“Kwa nini uogope sheria yenye kutoa adhabu kali iwapo wewe si mkosaji na wala hutarajii kutenda kosa,” alihoji.
Kwa upande wake Raismstaafu wa MCT, Jaji Dk. Robert Kisanga  alisema miongoni mwa changamoto zinazoikabili bodi  ni pamoja na wamiliki wa vyombo vya  habari kuvitumia kwa maslahi yao binafsi jambo ambalo si sahihi.
Mbali na wamiliki pia kitendo cha baadhi ya waandishi wa habari kuandika habari kulingana na matakwa ya wamiliki na si jamii, hivyo alisema kuna hajja ya kuvinoa ili viweze kufanya kazi zake kulingana na kanuni za taaluma ya habari.
Wajumbe wapya wa bodi ya MCT ni Rais mpya wa MCT, JJaji Thomas Mihayo, Hassan Mitawi ambaye ni makamu wa Rais na mwenyekiti wa  kamati ya fedha na utawala, Jaji Juxon Mley ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya maadili, Badra Masoud ambaye ni mjumbe wa kamati ya fedha na utawala na Rose Mwalimu .
Wengine ni Profesa Bernadeta Kilian, Wallec Maugo ambaye atakuwamjumbe katika kamati zote mbili ya fedha na utawala pamoja na ya maadili, Ally Mufuruki ambaye atakuwa mwenyekiti wa kamati ya fedha na utawala na Tuma Ally atakuwa katika kamati ya maadili.
@@@

No comments:

Post a Comment