WIZARA ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
imewataka wananchi kushirikiana na Serikali katika kulinda mkongo wa Taifa
kwani kumekuwa na desturi ya baadhi yao kuuchimba wakidhani wanaweza kupata
chuma chakavu.
Mbali na
hilo imesema kwamba mkongo huo umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za
mawasiliano ambapo awali gharama za intaneti zilikuwa 36000/GB hadi 9000GB
mwaka jana.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Afsa uhusiano wa Wizara hiyo Prisca
Ulomi alisema kwamba ni jukumu la kila mwananchi kuutunza mkongo huo ambao
umegharimu fedha nyingi za Serikali kwani ni wetu sote.
Alisema
Mkongo huo ambao kwa sasa wanaingia katika awamu ya tatu ukikamilika utasaidia
watoa huduma kufikisha huduma za mawasiliano
haraka na uhakikika na kwa gharama nafuu.
“Hata hivyo
itaharakisha maendeleo ya Taifa kwa kuwa wananchi watapata fursa ya kutumia
TEHAMA katika juhudi za kupambana na umaskini na kujiletea maendeleo kwa kasi
zaidi ambapo hadi sasa inaonyesha kwamba asilimia 10 ya matumizi ya Tehama
nchini yanachangia kwenye pato la Taifa kwa kiasi cha asilimia 1.38.
“Pia Mkongo
wa taifa unatoa muunganisho wa mawasiliano kwa nchi zote za jirani hasa zile
ambazo hazipakani na bahari ikiwa ni pamoja na Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi,
Zambia na Malawi, pia mkongo umeiunganisha Tanzania na Mikongo ya baharini ya
SEACOM na EASSY”alisema.
No comments:
Post a Comment