Monday, 1 September 2014

Hatimaye malalamiko ya wafanyabiashara wa Machinga Complex kuanza kufanyiwa kazi ikiwa pamoja na kujengwa kwa kituo cha daladala



MKUU wa mkoa wa Dar es Salaam,Said Mek Sadik amewaidi wafanyabiashara wa machinga Complex kujenga kituo cha daladala ikiwa ni moja ya  malalamiko yao ya muda mrefu.

Hatua hiyo ya kuahidi kujenga kituo hicho imekuja baada ya wafanyabiashara hao kutaka kuandamana kwa madai ya kuhitaji maelezo kutoka kwa Meya wa Almashauri ya Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa,  juu ya kiasi cha milioni 250   zilitolewa na TAMISEMI kwa matumizi ya kujenga kituo hicho cha daladala.

Akizungumza na mwandishi wa MTANZANIA Mwenyekiti wa wafanyabiashara hao Abubakar Rakesh alisema kuwa wamesitisha kuandamana kutokana na Mkuu wa mkoa kutoa ahadi ya kuanza  ujenzi ndani ya wiki moja na kuwataka wawe watulivu.

“Tulishajiandaa  kuandamana hadi  ofisini kwa Meya kama tulivyoahidi  wiki iliyopita lakini tulipata ujumbe kutoka kwa Mkuu wa Mkoa na kutuita ofisini kwake na baada ya kumueleza tulichokusudia akafanya mawasiliano na viongozi  wa Manispaa ya Ilala na kutuahidi ndani ya wiki moja ujenzi utaanza,”alisema Rakesh.

Alisema baada ya kamati ya mipango miji itakaa kikao leo na cha kuamua kazi hiyo ya ujenzi itaanza lini  ikiwa  mkandalasi  alikuwa  anataka kiasi cha shilingi Milioni 350 huku zilizokuwepo ni  Milioni 250 lakini aliaidi kuongeza na kufikia fedha zilizokuwa zinaitajika.

 Ikumbukwe kuwa madai ya wafanyabiashara hao yanakalibia miaka minne sasa tangu walipoanza kulala mika kuhusu miundo minu ya jengo hilo pamoja,lakini kukwazo kikubwa kilidaiwa ni Meya wa Almashauli wa Manispaa wa Ilaa na baadae wakakutana na Waziri mkuu ndipo mwanzoni wa mwaka huu kiasi cha shilingi Milioni 250 zilitumwa na TAMISEMI kwenda Manispaa ya Ilala ambapo  mpaka sasa matumizi ya fedha hizo hayaonekani.

No comments:

Post a Comment