Wednesday, 3 September 2014

Bilion 7.4 kutumika kujengea makuu ya bohari ya dawa




JUMLA ya shilingi billion 7.4 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Makao Makuu wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ujenzi unaotarajiwa kukamilika mwanzoni mwaka 2015.

Mbali na fedha hizo mpaka sasa tayari ujenzi huo umekamilika kwaasilimia 51 huku kiasi cha shilingi bilioni 3.7 kimeshalipwa ikiwa ni shemu ya utoaji wa fedha za ujenzi wa jengo hilo.

Akizungumza na Mtanzania Meneja Utawala wa (MSD) Johnson Mwakalitoko alisema
jengo hilo lenye ghorofa nne linalojengwa na kampuni ya China Railway Jianchang Engeneering CO. T Limited litakuwa na ofisi za watumishi, vyumba vya mikutano mikubwa na ya kawaida, maktaba, chumba cha kuhifadhia nyaraka muhimu za kumbukumbu, eneo maalumu la kuegeshea magari pamoja na eneo jingine kwaajili ya kuhifadhi mapipa ya maji.
Alisema kutokana na shuguli za ujenzi kwenda kwa haraka ni matarajio yao kwamba januari 2015 ofisi hiyo ityakuwa imeshakamilika.

Kwa upande Mwenyekiti Bodi Prof. Idris Mtulia ameipongeza menejimenti ya MSD kwa kazi hiyo ya ujenzi na kuiagiza menejimenti kuhakikisha ujenzi unasimamiwa kikamilifu ili uweze kukamilika katika muda uliopangwa kwenye mkataba.

“Imekuwa ni kawaida kwa kampuni za ujenzi kuahidi ujenzi utakamilika katika kipindi fulani mwisho wa siku haukamiliki hiyo si halali kabisa,ni vyema kuwa makini na kukamilisha ujenzi kwa wakati,”alisema Mtulia.

 Mwishoo.

No comments:

Post a Comment