Wednesday, 3 September 2014

Danny Welbeck reveals he dreamed of playing for Arsenal while he was still at Manchester United




Danny Welbeck has admitted dreaming of playing for Arsenal even before his £16million deadline-day move to the Emirates Stadium from Manchester United.
Welbeck revealed in and that he had always admired his new club's style from afar and pledged to capitalise on service from the Gunners' 'magnificent' midfield.
The England forward also expressed his delight that the transfer had 'finally' gone through.

'It's exciting times for me,' he said. 'It's great to be a part of this club and it's a team that I've always watched in the Premier League. I've envisaged myself playing in this team before. For it to finally happen is very exciting.'  
Welbeck undoubtedly has huge potential but still has plenty to prove after a meagre goalscoring return during his time at Old Trafford. 
The England forward notched just 29 goals in 142 first-team appearances for United, albeit with many of those coming from the substitutes bench or while shunted out on the wing playing a support role to Robin van Persie and Wayne Rooney.
The 23-year-old has craved a genuine opportunity to prove himself as a top-class central striker, which he should now get at Arsenal with Olivier Giroud out for four months with an ankle injury. And Welbeck has promised that he can be a roaring success while feeding off chances created by the likes of Alexis Sanchez, Jack Wilshere and Mesut Ozil.
'I believe the style of play the manager's got and the boys play and with the magnificent players in midfield slotting balls through, I can run on to the end of those balls and slot them away,' said Welbeck.

TTCL wabainisha mkongo wa mawasiliano umepunguza gharama za mawasiliano kutoka 36000/gb mwaka jana hadi 9000/gb mwaka huu



WIZARA  ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia imewataka wananchi kushirikiana na Serikali katika kulinda mkongo wa Taifa kwani kumekuwa na desturi ya baadhi yao kuuchimba wakidhani wanaweza kupata chuma chakavu.
Mbali na hilo imesema kwamba mkongo huo umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza gharama za mawasiliano ambapo awali gharama za intaneti zilikuwa 36000/GB hadi 9000GB mwaka jana.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Afsa uhusiano wa Wizara hiyo Prisca Ulomi alisema kwamba ni jukumu la kila mwananchi kuutunza mkongo huo ambao umegharimu fedha nyingi za Serikali kwani ni wetu sote. 
Alisema Mkongo huo ambao kwa sasa wanaingia katika awamu ya tatu ukikamilika utasaidia watoa huduma kufikisha huduma za mawasiliano  haraka na uhakikika na kwa gharama nafuu.
“Hata hivyo itaharakisha maendeleo ya Taifa kwa kuwa wananchi watapata fursa ya kutumia TEHAMA katika juhudi za kupambana na umaskini na kujiletea maendeleo kwa kasi zaidi ambapo hadi sasa inaonyesha kwamba asilimia 10 ya matumizi ya Tehama nchini yanachangia kwenye pato la Taifa kwa kiasi cha asilimia 1.38.
“Pia Mkongo wa taifa unatoa muunganisho wa mawasiliano kwa nchi zote za jirani hasa zile ambazo hazipakani na bahari ikiwa ni pamoja na Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia na Malawi, pia mkongo umeiunganisha Tanzania na Mikongo ya baharini ya SEACOM na EASSY”alisema.


Mambo husiyo yajua kuhusu Mario Mandzukic




Muda simrefu  mashabiki  wa mpira watafahamu kwanini  Diego Semeone alimuuza Diego Costa na kumsajili Mario Mandzukic (27), na Antonio Griezmann ili kuimarisha  safu ya  mshambuliaji  wa timu yake ya   Atletico Madrid.
Mandzukic amefanikiwa kuanza vyema baada ya kuifungia klabu yake bao la ushindi na kuweza kunyakuwa kombe la Super Cup baada ya Atletico kuifunga bao 1-0 timu  ya Real Madrid.
 Akithibitisha  ubora wake  na mafanikio makubwa aliyoyapata katika timu ya Bayern Munich ambapo amefanikiwa kuwa bingwa wa Ulaya 2013/14 akiwa katika timu hiyo kwa kutoa mchango mkubwa baada ya kufunga bao ambalo liliisaidia timu yake na kufanikisha ubingwa huo.
Bao hilo liliweza kumsahwishi kocha wa timu hiyo Pep Guardiola kujenga imani na mshambuliaji huyo kwa kuifunga  timu ya Borussia Drtmund. 
MAISHA YAKE
Mandzukic amezaliwa Mei 21/1986 katika mji mdogo uliopo ndani ya nchi ya Croatian uitwao Slavonski Blod  ukiwa umepakana na mpaka wa Bosnia  huku mji huo ukiandamwa na vita vya mara kwa mara vya mwaka 1992 na hatimaye  familia ya mshambuliaji kuamua kuhama ikiongozwa na baba yake mzee Mato alinukuliwa akisema “kitu cha msingi kwa familia yangu  ni usalama,eneo hili tunashuhudia kila siku watu wakifa kwa vita inayoendelea  kutokana na hali hiyo hatuwezi kuendelea kuwepo hapa  hatuwezi hata kidogo tunatakiwa kuondoka ili kuyanusuru maisha yetu,”.
HARAKATI ZAKE  KATIKA SOKA.
Baada ya kuondoka Crotia katika harakati za kutafuta usalama ndipo safari ya familia yake  ikafika  eneo la Ditzingen Ujerumani karibu na mji wa Stuttgart  hapo ndipo kipaji cha mshambuliaji huyo kikaanza kuonekana na alipofika miaka sita baba yake anayejulikana kwa jina la  Mato akaamua kumpeleka katika kituo cha  mpira cha watoto cha TSF Ditzingen na kufanikiwa kujiunga.
  
SAFARI YAKE YA KURUDI CROTIA
Mwaka 1996 familia yao ilikataliwa kupata ruhusa ya  kuendelea kuishi katika ardhi ya Ujerumani na kutimkia katika visiwa vya Baklans pembezoni mwa nchi hiyo ambapo ilipokonywa umiliki wa eneo hilo baada ya vita vya pili vya dunia.
Hata  hivyo  mshambuliaji huyo na mipango yake kucheza mpira akiwa katik timu ya NK Marsonia kabla ya kurudi Crotia na kujiunga na timu ya NK Zagred  baadae msimu wa usajili wa 2007 akafanikiwa kujiunga na timu kubwa Dinamo Zagreb kwa pauni milioni 1.3 baada ya kuuzwa mshambuliaji wa timu hiyo Eduardo da silva  .
KIPINDI KIZURI KATIKA MAISHA YAKE
Baada ya  Edin Dzeko kujiunga na Man City Januari 2011,ndipo nyota ya Mandzukic ikaanza kungaa katika timu hiyo ya Wolfsburg akithibitisha kipaji chake msimu wa 2011/12 akifunga mabao 12 na kutoa pasi 10 zilizo kuwa na matokeo ya mabao, akimaliza  huku akitajwa kuwa mmoja wa wafungaji bora wa mashindano ya Euro 2012  na kupelekea   timu  kubwa kama Bayern Munich kumuhitaji ambapo  Rais wa timu hiyo Uli HeneB alisikika akisema “timu yetu inatakiwa tuwe na mshambuliaji kama Mandzukic kwa napenda anavyo cheza” na kupelekea kusajiliwa baada ya timu yake ya taifa kutolewa na Ukraine katika mashindano  ya Mataifa   yaliokuwa yakifanyika nchini Poland.
SUPER MARIO WANAKUTANA
Katika msimu 2011/12  Mandzukic  alifanikiwa kuifungia timu yake ya taifa na klabu jumla ya mabao 45 na  kukaribisha ushindani mkali kutoka kwa Mario Gomez ambaye kwa kipindi hicho alikuwa ndio mshambuliaji  namba moja wa  timu hiyo.
Kitendo cha kuumia kwa Gomez kikafungua ukulasa mpya kwa Mandzukic na kupelekea kuwa mshambuliaji wa kutegemewa katika timu hiyo huku akionyesha uwezo mkubwa katika Supercup dhidi ya Dortmund  na kumfanya Gomez asubili katika benchi akingoja aingie kama mchezaji wa akiba akimaliza ligi akiwa  na mabao 15.

ANAYEVUTIWA NAE ZAIDI
Akiwa katika timu ya NK Marsonia pamoja na  Ivica Olic ambaye wanacheza timu moja ya Crotia pia akicheza katika timu ya Hertha Berlin na Hamburger  SV kabla ya kujiunga na Bayern 2009 na Mandzukic akumtaja Olic kuwa ndiye anamvutia zaidi katika suala zima la uchezaji mpiara hali ilipelekea Mandzukic kukili kuwa akisema “Najua alikuwa akipendwa na mashabiki hapa ,”na kuongeza kuwa Olic alikuwa akifanya juudi kubwa kuakikisha anakuwa bora wakati wote  hivyo angependa kufanya alichofanya akiwa na timu hiyo.

MAPENZI YAKE KWA TIMU ZA UJERUMANI
Miaka minne aliyotumia akiwa  katika timu ya Baden- Wurttemberg ilimfanya kupenda kuendelea kuishi katika nchi ya Ujerumani  na kupelekea kukataa kujiunga na baadhi ya timu kutoka England na Ufaransa  kipindi cha usajili 2010 na kujiunga na Wolfsburg na baadae   Bayern 2012 akisema “Ujerumani ni nyumbani pia najiisi fuaraha nikiwa hapa ”.

MALENGO YAKE
Ili mshambuliaji aweze kuwa katika kiwango bora na kuzivutia baadhi ya timu kubwa ni mara nyingi anapimwa katika uwezo wake wa kufunga  mabao lakini Mandzukic ameonyesha ubora wake katika hilo na kutengeza nafasi nyingi za mabao na kufanikiwa na kila kitu kinachotakiwa katika kucheza mpira akiwa kama mshambuliaji.

“Najiona mpya kila nikiwa uwanjani endapo  nikiwa nje ya uwanja najiisi bado naitaji kupambana ili kushinda na kuleta changamoto,”alisema Manduzukuic.

MAISHA BINAFSI

Nimshambuliaji ambaye hapendi kuwa karibu na vyombo vya ukilinganisha na wengine kwani maisha yake yamekuwa tofauti akiwa na mpenzi wake Ivana na mbwa wake kipenzi Lene huku akitembelewa mara kwa mara na dada yake Ivana aliyeamia
ujerumani 2007 mwenye jina linalo fanana na mpenzi wake.

Bilion 7.4 kutumika kujengea makuu ya bohari ya dawa




JUMLA ya shilingi billion 7.4 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Makao Makuu wa Bodi ya Wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD) ujenzi unaotarajiwa kukamilika mwanzoni mwaka 2015.

Mbali na fedha hizo mpaka sasa tayari ujenzi huo umekamilika kwaasilimia 51 huku kiasi cha shilingi bilioni 3.7 kimeshalipwa ikiwa ni shemu ya utoaji wa fedha za ujenzi wa jengo hilo.

Akizungumza na Mtanzania Meneja Utawala wa (MSD) Johnson Mwakalitoko alisema
jengo hilo lenye ghorofa nne linalojengwa na kampuni ya China Railway Jianchang Engeneering CO. T Limited litakuwa na ofisi za watumishi, vyumba vya mikutano mikubwa na ya kawaida, maktaba, chumba cha kuhifadhia nyaraka muhimu za kumbukumbu, eneo maalumu la kuegeshea magari pamoja na eneo jingine kwaajili ya kuhifadhi mapipa ya maji.
Alisema kutokana na shuguli za ujenzi kwenda kwa haraka ni matarajio yao kwamba januari 2015 ofisi hiyo ityakuwa imeshakamilika.

Kwa upande Mwenyekiti Bodi Prof. Idris Mtulia ameipongeza menejimenti ya MSD kwa kazi hiyo ya ujenzi na kuiagiza menejimenti kuhakikisha ujenzi unasimamiwa kikamilifu ili uweze kukamilika katika muda uliopangwa kwenye mkataba.

“Imekuwa ni kawaida kwa kampuni za ujenzi kuahidi ujenzi utakamilika katika kipindi fulani mwisho wa siku haukamiliki hiyo si halali kabisa,ni vyema kuwa makini na kukamilisha ujenzi kwa wakati,”alisema Mtulia.

 Mwishoo.