Labels
Showing posts with label Entertainment. Show all posts
Showing posts with label Entertainment. Show all posts
Friday, 8 August 2014
Wema sepetu afunguka kuhusu kuzaa..........!!
Wema Leo Ameamua Kuwafungukia Wale
wanaopenda kumforce azae, Wema aliweka Picha ya Kim Kardashian akiwa
amembeba Mtoto wake na Kuandika Mbona Huyo Kazaa akiwa Miaka ya 30 sasa
kwanini watu wanamforce wakati yeye bado yupo 20′s Jisomee Mwenyewe hapo
chini:
Jack Wolper adaiwa kutibua Uchumba wa Nay Wa Mitego na Siwema
Mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ amefungukia madai ya kutoka na msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper na kudai kuwa wao ni washikaji tu ila ukaribu wao umesababisha mtifuano kati yake na mchumba wake, Siwema.
Mahojiano kati ya mwandishi wetu na Nay yalikuwa hivi:
Mwandishi: Kuna madai kuwa wewe unatoka na Wolper, hii ikoje?
Nay: Wolper ni mshikaji wangu, kama watu wanavyojua kwamba yule ana mambo ya kisela f’lani na hicho ndicho kinanifanya nimpende.
Nay: Wolper ni mshikaji wangu, kama watu wanavyojua kwamba yule ana mambo ya kisela f’lani na hicho ndicho kinanifanya nimpende.
Ila
najua kitu kilichowafanya watu wahisi kuna kitu kati yangu na yeye ni
baada ya kuposti picha yangu kwenye ukurasa wake wa Insta na hapo ndipo
likaibuka tatizo. Na hilo lilileta ugomvi kwenye uhusiano wangu lakini
ukweli ni kwamba kama mahusiano yapo ni ya kawaida tu.
Mwandishi: Sasa wewe na Wolper mkikutana huwa mnazungumzia nini?
Nay: Mambo ya kazi tu, si unajua nina mpango wa kucheza muvi baadaye
Mwandishi: Mbona sasa inadaiwa mnatoka kwa siri?
Nay: Mambo ya kazi tu, si unajua nina mpango wa kucheza muvi baadaye
Mwandishi: Mbona sasa inadaiwa mnatoka kwa siri?
Nay: Hayo maneno ya watu tu japokuwa ni mwanamke mzuri, anamvutia mwanaume yoyote rijali
Mwandishi: Ikitokea ameingia mzimamzima kwako itakuwaje?
Nay: Ikitokea ameamua kuingia mzimamzima, nitaangalia mapokeo yake (Kicheko sanaaa)
Nay: Ikitokea ameamua kuingia mzimamzima, nitaangalia mapokeo yake (Kicheko sanaaa)
Mwandishi alifanya jitihada za kumsaka Wolper kupitia simu yake ya mkononi lakini hakuweza kupatikana.
Thursday, 7 August 2014
Anti Ezekiel afunguka kuhusu kutoka na dansa wa Diamond
Mwanzoni mwa wiki hii miongoni mwa stori ambazo zilitoka na kuenea kwenye magazeti kadhaa ni pamoja na inayomhusu Anti Ezekiel kusemekana kuwa anatoka na dansa wa Diamond Platnumz.
Taarifa ya awali ilidai kuwa mpenzi huyo wa dansa wa Diamond alienda kufanya vurugu nyumbani kwa Anti Ezekiel,Anti Ezekiel kapatikana na kaongelea mahusiano yake na Moses Iyobo ambaye ndiye dansa wa Diamond Platnumz.
Ali Kiba ampa ushauri Tunda Man baada ya kuugua ghafla
Mwimbaji
wa Tip Top Connection, TundaMan aliwashangaza wengi baada ya kueleza
kuwa alipokea simu yenye namba nyingi asizozielewa na ghafla akapata
mshtuko na kuishiwa nguvu, hali iliyomsababisha akimbizwe hospitali
ambapo alipewa matibabu.
Licha
ya kuwa wataalam na mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) walieleza
wazi kuwa kitaalam simu haiwezi kabisa kuwa chanzo cha tatizo hilo,
TundaMan alisisitiza kuwa yeye ndiye aliyepata tatizo na anajua
kilichotokea.
“Wao wanasema haiwezekani kwa sababu hilo tatizo halikuwakuta…lakini kwa kuwa mimi ndiye nimekuwa affected kwa siku mbili tatu, mimi naamini kuwa tukio hilo lipo na limekuja baada ya kupokea ile simu. Wao wanaongea kitaalam siwezi kubishana nao, lakini mimi limenikuta na nimeona.” Amesema Tundaman
Kutokana
na sintofahamu hiyo, Tundaman ameeleza kuwa msanii mwenzake, Ali Kiba
alimshauri kwenda katika nyumba ya ibada ili apate dua maalum.
“Yeah
inawezekana (ni ushirikina) kwa sababu vitu kama hivyo huwa vinatokea
sana na ndio maana ndugu yangu Ali Kiba amenishauri nikapate dua.” Amesema Tunda Man.
Ameeleza kuwa tayari amechukua uamuzi huo ingawa hali yake pia inaendelea kuimarika baada ya kupata matibabu.
Wiz Kid amjibu Davido kupitia twitter
Wednesday, 6 August 2014
Aunt Ezekiel anusurika kupigwa nyumbani kwa Wema
Staa
wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson anadaiwa kukinukisha
nyumbani kwa Wema Isaac Sepetu baada ya kunusurika kufumaniwa na mume wa
mtu, Moses Peter Iyobo a.k.a Moze Iyobo ambaye ni densa wa Nasibu Abdul
‘Diamond’.
Habari
za kuaminika zinadai kwamba tukio hilo lilitokea hivi karibuni nyumbani kwa Wema, Kijitonyama, Dar ambapo Aunt alisababisha
tafrani iliyosababishwa na mke wa mwanaume huyo aliyetajwa kwa jina la
Mwengi Ally.
Kwa
mujibu wa mashuhuda wetu waliokuwa wakizungumza kwa kupokezana, Mwengi
alidai kwamba Aunt amekuwa akitembea na mumewe huyo hivyo timbwili
lilianzia nyumbani kwa Aunt, Mwananyamala A jijini Dar.
Ilidaiwa
kwamba, huku Aunt akiwa hajui hili wala lile, ghafla waliibuka
wasichana saba na kumuanzishia mwigizaji huyo.Mashuhuda hao walidadavua
kwamba katika kujinusuru na kipigo ambacho alihisi akiwa peke yake,
angeumizwa Aunt alikimbilia nyumbani kwa shoga yake, Wema.
Ilidaiwa
kwamba wasichana hao hawakuishia hapo kwani walimkimbiza Aunt hadi
wakamuona akiingia kwa Wema ambapo walipofika getini walikutana na
meneja wa msanii wa Bongo Fleva, aitwaye Mirrow, Petit Man ambaye
walimuomba amtoe Aunt ili wamshikishe adabu ajifunze kukaa mbali na
waume za watu.
Ilisemekana
kwamba katika tafrani hiyo getini, Wema alitoka na msichana wake
aitwaye Careen lakini Aunt hakutoka ambapo waliwaambia wasichana hao
kuwa Aunt hawezi kutoka na isitoshe wa kulaumiwa ni Moze Iyobo kwani
yeye ndiye anayedaiwa kumtongoza Aunt na kuanza kuchati naye hadi mkewe
akanasa meseji zao za mapenzi.
Baada
ya kujazwa data hizo, Mwandishi alimtafuta Mwengi ili kupata maelezo ya
kina kuhusiana na ishu hiyo ambapo alikiri kwenda kwa Aunt na Wema
lakini hakufanikiwa kumpata Aunt kwani kama angemkamata, maafa
yangetokea.Mwengi alisema kuwa siku ya tukio aliitwa na Aunt maeneo ya
Mlimani City, Dar na akamwambia aende na mtoto akamfanyie shopping.
Alisema
baada ya kuambiwa hivyo hakuwa na hiyana kwani alijua kuwa ni kama mama
yake mkubwa na shoga wa mpenzi wa baba yake mkubwa ambaye ni Diamond,
kumbe nyuma ya pazia kulikuwa kuna kitu kingine kimejificha.“Niliporudi
nyumbani, mume wangu aliniambia nimpige picha kwa kutumia simu yake,
nilipoifungua ndipo ikaingia meseji kutoka kwa Aunt.
“Nilipoisoma
ile meseji nikagundua kuwa walianza kuchati muda mrefu kuhusu mapenzi
yao, ndipo nikakusanya jeshi langu na kumfuata nyumbani kwake
nikamshikishe adabu, amshukuru Wema kumficha maana sipati picha kwa
jambo ambalo lingetokea. Ingekuwa mwisho wake wa kupora waume za watu,” alisema Mwengi.
Alipotafutwa Aunt na kuulizwa juu ya sakata hilo, alijibu kwa kifupi: “Sina muda mchafu wa kuongea halafu nimelala, kwa sasa niache nipumzike.”
Rose Mhando anatamani kuwa na Gwajima.......!
Nyota
wa nyimbo za Injili nchini, Rose Muhando amesema anatamani sana kuhamia
kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mchungaji Josephat Gwajima
kutokana na mahubiri yake mazuri.
“Natamani
nihamie katika kanisa la Mchungaji Gwajima lakini mimi huwa napenda
kumuita Askofu kwa sababu ya upako alionao, naomba ikiwezekana na mimi
nihamie hapa,” alisema Rose.
Monday, 4 August 2014
EXCLUSIVE: Chris Brown akana kutemwa na Karrueche .......!!!!!!!!!!!!
Kutokana
na tetesi kwamba
Chris Brown katemwa na aliyekuwa mpenzi wake Karrueche, madai hayo ameyakanusha na kusema kuwa yeye ndiye
aliye mtema kimwana huyo.
Taarifa
kutoka vyanzo mbalimbali ambavyo vipo karibu na wapenzi hao zinasema kuwa Chris alishtushwa na habari zilikuwa kuwa
zimeenea kwamba yeye kuachwa na Karrueche badala yeye kumuacha.
Taarifa hizo zilipo takiwa kutaja Sababu
zinazodaiwa kuachwa kwa karrueche zinasema kuwa
Chris alipogundua Karrueche alikuwa akichati na mwanaume mwingine
na kutumiana picha wakati wakiwa pamoja mara.
Taarifa
hiyo ilidai kuwa Brown alipatwa na hasira baada ya mwana dada huyo kufanya
mahojiano katika maonyesho ya mavazi yake na kuzungumzia juu ya uhusiano wao
Ikumbukwe Karrueche alinukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari huko Marekani ivi karibuni akisema kwamba licha ya Chris kuendelea kuwa karibu na Rihhana lakini kinacho muhudhi zaidi ni kwamba bado anavitendo vya kitoto na kuendekeza sana bata na wanawake kuliko shughuli zake za muziki kitu ambacho amekichoka.
Ali Kiba: Lulu Michael anafaa kuwa MKE
Kwa
mara ya kwanza, staa anayeitikisa nchi kwa sasa na wimbo wake wa Mwana,
Ali Kiba amefunguka kuwa mwigizaji kiwango Bongo, Elizabeth Michael
Kimemeta ‘Lulu’ anafaa kuwa mke (wife material) huku akiweka wazi sifa
kibao alizonazo.
Kiba
ambaye hivi karibuni ameibua mijadala mingi katika mitandao ya kijamii,
usafiri wa umma na kwenye baa juu ya ujio wake mpya akisemekana kurudia
kiti chake ambacho alikikalia Mbongo Fleva, Abdul Nasibu ‘Diamond’ kwa
muda, mwaka 2010 aliwahi kuripotiwa kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na
Lulu ambaye wakati huo alikuwa na umri chini ya miaka 18!
LULU ANAFAA KUWA MKE
Akizungumza
na Globa TV Online mwishoni mwa wiki iliyopita, Kiba alisema Lulu
anafaa kuwa mke kwa vile ni mchapakazi sifa ambayo mke mwema anapaswa
kuwa nayo.
AMMWAGIA SIFA
Kiba
alisema Lulu anajua kuhangaika, anajua kupambana kusaka pato lake
kihalali kupitia mauzo ya sinema zake anazozizalisha kitu ambacho
kinawashinda mabinti wengi na kuangukia katika biashara ya kuuza miili
(ukahaba).
Licha
ya kummwagia sifa hizo, kipindi hicho alichokuwa akitajwa kuwa naye,
Lulu alikuwa na matukio ambayo hayakuwa na maadili lakini Kiba hayo
hakuyatilia maanani.
Mwandishi: Unafikiri Lulu ni ‘wife material’ (mke mwema) ambaye unaweza kumweka ndani akalea watoto na kuijenga familia bora?
Kiba: Yeah! Anafaa kuwa mke, ni binti anayejituma, mchapakazi, mtafutaji. Kwangu mimi mtu wa namna hiyo ndiyo anafaa kuwa mke.
Mwandishi: So, unataka kutuambia kwamba unaweza kumuoa?
Kiba: Sijasema hivyo mimi, nimesema anafaa kuwa mke.
ACHOMOA KUBANWA KISHERIA
Licha
ya kuchomoa ishu hiyo ya uhusiano, waandishi wetu walimbana zaidi staa
huyo afafanue kwa nini alitajwa yeye na si msanii mwingine huku ikidaiwa
kuwa, Lulu hakuwa ametimiza miaka 18 hivyo kubanwa kisheria (ya watoto
na kujamiiana).
“Sijatembea
naye ndiyo maana unaona hata sheria haijanihukumu, endapo ningekuwa
nimetembea naye, basi sheria ingeweza kunitia hatiani na ningefungwa
jela,” alifafanua Kiba.
AWASHANGAA WANAOMSHANGAA
Kiba aliongeza kuwa, anashangaa sana kuona watu wanamsema vibaya yeye kupendwa na Lulu.
“Lulu
ni msanii mwenzangu, anapenda kazi zangu na mimi napenda za kwake. Ni
rafiki wa kawaida, hakuna kitu kingine cha ziada. Nawashangaa wanaozusha
ya kuzusha, hivi kwani kuna tatizo Lulu akinipenda? Sidhani kama ni
kosa, ana haki ya kunipenda kutokana na muziki wangu.
“Unajua
muziki mzuri huwa unapenya automatically, huwezi kuzuia hisia za
muziki, mtu unaweza ukawa humpendi msanii f’lani lakini ukapenda muziki
wake, unajikuta tu unampenda, unaanza kuimba nyimbo zake,” alisema Kiba.
KUMBUKUMBU MBICHI
Juzikati
wakati Kiba anatambulisha nyimbo zake mbili kwa mpigo (Mwana na
Kimasomaso), Lulu, kupitia mtandao wa Instagram alitupia maneno ya
kummwagia sifa staa huyo, liliibuka kundi ambalo linatajwa kuwa ni
wafuasi wa mwigizaji Wema Sepetu ‘Team Wema’ na kuanza kumshambulia kwa
maneno machafu.
KIBA AFUNGUKA
Akizungumzia
ishu hiyo, Kiba alisema waliofanya hivyo hawakumtendea haki Lulu kwani
ana haki ya kueleza hisia zake pale anapoguswa na muziki mzuri.
“Hawajatenda haki kwa sababu Lulu ni binadamu kama walivyo wengine, ana haki ya kupenda kitu kizuri,” alisema Kiba.
KUHUSU KIFO CHA KANUMBA
Kiba
akizungumzia juu ya kuhusishwa na kifo cha aliyekuwa nyota wa sinema
Bongo, marehemu Steven Kanumba ambapo alidaiwa kunaswa kwa meseji za
mapenzi alizozituma kwa Lulu ndiyo zilizosababisha mtifuano ambao
ulisababisha kifo cha Kanumba, alikana madai hayo.
“Si
kweli, sikuwa nimewasiliana na Lulu siku hiyo kabla ya tukio. Nakumbuka
nilikuwa safarini, baada ya tukio nilimpigia Lulu kutaka kujua ukweli
wa taarifa za kifo kwa sababu marehemu alikuwa mtu wangu wa karibu kama
alivyo Lulu,” alisema Kiba.
AMGUSIA WOLPER
Kwenye
mahojiano hayo, mkali huyo alizungumzia ishu ya mwigizaji, Jacqueline
Wolper kukiri kwamba Kiba ndiye mwanaume aliyemtoa usichana wake kwenye
simulizi iliyochapishwa katika Gazeti la Championi hivi karibuni.
Saturday, 2 August 2014
Shilole na NUH wanaswa Live Chumbani Akingonoka
Picha za staa wa sinema na Bongo
Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole Kiuno’ zinazomuonesha live akiwa chumbani
tena kitandani kimahaba na mwandani wake, Nuh Mziwanda zimevuja….
Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho ni mtu wa karibu wa Shilole, picha
hizo walijipiga wenyewe wakiwa kitandani nyumbani kwa mwanadada huyo,
Kinondoni jijini Dar.
Chanzo hicho kilidai kwamba picha hizo
walijipiga baada ya kumalizika kwa Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani
kwani kabla ya hapo wasingefanya hivyo.
Katika picha hizo zinazowaonesha wawili
hao wakiwa katika mahaba niue, Shilole anaonekana akiwa amemlalia
Mziwanda ambaye naye amejiachia vya kutosha.
Habari za ndani zinadai kwamba mmoja wa
watu wa karibu alishika simu ya Shilole kisha akajifowadia picha hizo
ndiyo chanzo cha kumfikia mtu wetu huyo.
Baada ya kuzidaka picha hizo, mwandishi
alimtafuta Shilole ambaye kwa sasa anakimbiza na ngoma yake mpya ya
Namchukua ambapo alipopatikana kwa njia ya simu alisomewa mashitaka yake
ndipo akafunguka namna alivyochezewa na mtu wa karibu yake.
“Kweli
hizo picha ni zangu na Nuh (Mziwanda), tulijipiga kwa ajili ya
kumbukumbu na tulikuwa na muda mrefu hatujiachia si unajua tena Mwezi
Mtukufu?
“Unajua simu yangu haina
password na nina watu wengi wa karibu so nahisi ndiyo wamezivujisha na
nikimjua namtoa kabisa kwenye network yangu maana siku nyingine anaweza
kunifanyia jambo kubwa baya.”
Davido atangaza Ngoma mpya aliyomshilisha mkali kutoka Maybach Music Group
Skelewu, Gobe, Ekuro,One of a
kind,Aye ni baaadhi ya nyimbo ambazo zinamuweka Davido kwenye chati ya muziki
na kumsaidia kushinda tuzo mbalimbali kama BET,MTV na nyingine nyingi.
Wiki ijayo mashabiki wa Davido wanatajia
kupata kusikiliza nyimbo mpya kutoka kwa Davido akiwa pamoja na member wa MMG anayetambulika
kwa Wale. Wimbo unaitwa Won Le Ba na taarifa hii imeripotiwa na Davido
mwenyewe.
Friday, 1 August 2014
EXCLUSIVE:Karrueche Tran na Chris Brown kuachana
Vyanzo mbalimbali majuu vimeripoti yanayoendelea katika mahusiano ya Chris Brown
na mwana dada Karrueche vikisema Karrueche alishtukia mbinu chafu ya Chris hivi karibuni alipo "like"picha
mbili za shabiki kwenye Instagram ya
Rihanna wakati wakiwa pamoja.Hata hivyo Rihanna alikuwa ni sehemu ndogo ya matatizo yaliyojitokeza kwa Karrueche na Chris.
Taarifa hiyo inasema kuwa kwa muda mrefu Karrueche
alikuwa hana raha ...huku ikidaiwa kuwa kwa sababu Chris kuwa na vitndo vya
kitoto mara kwa mara na kutumia muda mwingi kupati kuliko kufanya shughulizake
za muziki
“Chris act immature,like child and he’s ruining his life
by spending more than making music”alinukuliwa Karrueche.
Vyanzo hivyo vya
habari vinasema kuwa vitendo vya chris vimekuwa vya kukatisha moyo.ikiwa wiki hii alikwenda St Tropez na
kumchukua ratokanae huku mwenyewe akiwa hajui.
Pia vyanzo hivyo vinasema kuwa Maamuzi ya Karrueche si jambo la wivu kwa kuwa aliamua kubadili namba ya simu yake ya zamani ili hasiweze kuwasiliana na Chris na inaweza kuchukuwa muda mambo kuwa sawa.
Subscribe to:
Posts (Atom)







