
Ndege
hiyo aina ya BA ilikuwa ikielekea
Heathrow Uingereza kutoka Dubai safari ambayo kwa kawaida huchukua saa saba
hadi kufika.
Abiria
mmoja aliyekuwa ndani ya ndege hiyo aliyejulikana kama Abhishek Sachdev, aliandika kwenye mtandao
wake wa kijamii wa Twitter kuwa
''Amini
usiamini ndege yetu ya British Airways imelazimika kurejea dubai baada ya
wahudumu kugundua kuwa harufu mbaya inatokea kwenye choo cha ndege hiyo.
“Yamkini
rubani wa ndege hiyo aliwaita msimamizi wa wahudumu wa ndege hiyo ndipo
tukang'amua kuwa kulikuwa na tashwishi katika safari yetu” Sachdev alinukuliwa
na gazeti moja.
Anasema
walielezwa na rubani kuwa harufu mbaya
ndani ya ndege hiyo inatokana na choo cha ndege hiyo kuwa kichafu na kwamba
ilikuwa ni ya kinyesi.
Sachdev
anasema hadi kufikia wakati huo ilikuwa takribani nusu saa tangu ndege hiyo
ipae angani hivyo ikalamika kujerea nchini Dubai na ikawapasa kusubili zaidi ya
saa 15 kwa kuwa hapakuwa na mbadala wa kurejea London.
Kwa upande
wake mwakilishi wa ndege hiyo Greg James, Sarah, aliiambia Radio 1 kuwa jambo hilo
halikuwa suala la kufanyiwa utani kwani ukiwa ndani ya ndege ni tishio kubwa
kwa afya ya rubani na abiria kwa jumla.''Ndani ya ndege huwa kunautupu wa hewa kwa hivyo asili mia 50 ya hewa inayotumika ni ileile kwa hivyo harufu mbaya ingeathiri vibaya afya ya abiria ndio sababu ndege hiyo haikuwa na budi ila kurejea iliisafishwe''.alisema.
Hata hivyo shirika hilo la ndege liliomba msamaha kwa usumbufu wowote kwa abiria wake walioathirika siku hiyo.
No comments:
Post a Comment