Tuesday, 17 March 2015

Kutazama video za ngono zawaponza Majaji 3 nchini uingereza




MAJAJI watatu nchini Uingereza  wamefutwa kazi kwa kutumia muda wao ofisini kutizama filamu za ngono.
Wakitajwa majina kuwa ni Jaji Timothy Bowles anayesikiza kesi za wilaya , jaji wa maswala ya uhamiaji Warren Grant na jaji Peter Bullock kuwa wamefutwa kazi.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa  idara ya mahakama walithibitisha kuwa Majaji hao walipatikana na hatia ya  kutumia mtandao rasmi wa mahakama hiyo.
 Maafisa hao wanasemekana kuwa Majaji hao walitazama mitandao yenye filamu za ngono huku wakifahamu vyema kuwa ilikuwa ni ukiukaji wa sheria za matumizi kwa mujibu wa msimamizi wa idara hiyo ya Mahakama.
Hata hivyo kiongozi wa idara ya mahakama hiyo ya Uingereza na jaji mkuu waliwapata na hatia ya kwenda kinyume cha maadili ya mahakama.
Jaji wa nne Andrew Maw aliamua kustaafu mwenyewe wakati uchunguzi huo ukiendelea badala ya kufikishwa kizimbani.
Mwandishi mmoja wa  maswala ya kisheria anayejulikana kama Clive Coleman  anasema kuwa makosa hayo yalikuwa makubwa sana katika mizani ya uadilifu wa majaji.
Aidha imefahamika kuwa hakuna hata mmoja wao atakayeruhusiwa kufanya kazi katika idara ya mahakama tena.

No comments:

Post a Comment