KATIKA muendelezo wa vituko
duniani harusi moja ilitibuka nchini India
baada ya bwana harusi kufeli swali rahisi sana la hisibati aliloulizwa na bi
harusi.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa kihoja
hicho cha aibu kinachosemekana kutokea wakati bi harusi alipomuuliza swali bwana harusi kwamba ‘15 ukiongeza 6 utapata
nini’ na bwana huyo hasijue cha kujibu.
Hata hivyo polisi katika jimbo hilo la
Uttar Pradesh nchini India wanasema kuwa sherehe za harusi hiyo zilitibuka
baada ya bi harusi kufoka mumewe mtarajiwa alipotoa jibu lake kuwa ''17 ''.
Ni mara nyingi maharusi hukutana kwa
mara ya kwanza katika sherehe za harusi yao.
Cha kushangaza ni pale bi harusi alikurupuka
na kuondoka jukwaani akiwa amenuna huku akisema
hawezi kuoa mtu ambaye hakwenda shuleni.Hivyo juhudi zote za ndugu na jamaa
pamoja na marafiki waliofika katika eneo hilo kushuhudia ziliambulia patupu.
Na baadae polisi katika jimbo hilo walisema
kuwa jamaa wa bwana na bi harusi wote walikubaliana kurejesheana zawadi zote
walizokuwa wametoa kwaajili ya wapendwa hao.
Ifahamike kuwa asilimia kubwa ya
ndoa zote nchini India hupangwa na wazazi na mara nyingi maharusi hukutana kwa
mara ya kwanza katika sherehe za harusi yao hivyo Baba yake bi
harusi Mohar Singh ambaye ndiye aliyekuwa amepanga harusi hiyo katika kijiji
cha Rasoolabad akiongea na waandishi alidai kuwa mwanawe alishangaa mumewe mtarajiwa Ram Baran hakuwa msomi.
Katika tukio
linalofanana na hilo nchini humo lilitokea mwezi uliopita bi harusi mwengine
aliolewa na mgeni katika harusi yake baada ya Mumewe aliyekuwa amepanga kumuoa
kuanguka kifafa dakika chache tu kabla ya wawili hao kuunganishwa kuwa mume na
mke .
No comments:
Post a Comment