Hali hiyo imetokana na agizo la Rais Jakaya Kikwete la kila shule ya sekondali ya Serikali iwe na maabara
ya Biolojia,Kemia na Fzikia huku Mkoa wa Dar es Salaam ukiwa na Shule za
Serikali 135 na kutakiwa kuwa na maabara 405.
Hayo aliyazungumza jana,jijini Dar es Salaam alipokuwa
akiongea na waandishi wa habari alisema hali hiyo imetokana na kuwapo kwa
mafundi wa wataalam wa maabara saba
katika shule 135 za sekondari.
Alisema kutokana na tatizo hilo Manispaa zitawajibika
kuwatafuta wataalam waliostaafu ili kuwaajili ikiwa lengo ni kupunguza uhaba
huo pamoja na kuharakisha ujenzi.
“Kutokana na uhaba huu watalaam watafutwe popote na
waajiliwe kutokana na ujuzi wao japokuwa jambo ili litakuwa gumu kwa upande wa
mikoani lakini mijini halitasumbua kwa kuwa baadhi yao wanaendelea
kujishughulisha na taaluma hiyo, ”alisema.
Aidha alisema kuwa miongoni mwa changamoto nyingine
zilizojitokeza ambazo zinadaiwa kuzotesha ujenzi huo pamoja na ukosefu wa
umeme, maji na mabeseni ya maabara.
Hata hivyo Mkuu huyo amesema kuwa ametoa maagizo kwa halmashauri
kutafuta ufumbuuzi wa changamoto hizo.
No comments:
Post a Comment