Saturday, 13 December 2014

TAMISEMO WATOA MAELEKEZO NA UTARATIBU WA KUFUATA SIKU YA KUPIGA KURA



WIZARA ya tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imetoa utaratibu wa kufuata siku ya kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwenye ngazi za vijiji,Mitaa, na Vitongoji.
Utaratibu huo utakaotumika katika siku ya upigaji kura,kuesabu na kutangaza matokeo, umeelekezwa na kufanunuliwa na kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa za Mwaka huu.
Hakitoa ufafanuzi juu ya utaratibu huo jana jijini Dar es Salaam,Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Jumanne Sagin alisema wizara imelazimika kutoa ufafanuzi huo ili kufahamisha Wananchi njia za kufuata katika kupiga kura na kupunguza hali ya sintofahamu.
“Siku hiyo patakuwa na karatasi ya kura ambayo itaandaliwa na halmashauri husika ikiwa na jina la mgombea,jina la chama,Nembo ya halmashauri,na mpiga kura atatakiwa kutia alama ya vema katika kisanduku kilichoko chini ya nembo ya chama ili kuonesha kuwa amempigia mgombea aliyemtaka,”alisema Sagin.
Alisema utaratibu wa kupiga kura utaanza saa mbili (2:00) asubuhi hadi saa kumi jioni ambapo wapiga kura watakao kuwapo kituoni saa kumi (10:00) jioni wataruhusiwa kupiga kura hadi watakapokuwa wamemalizika.
Alisema Msimamizi Msaidizi atajirizisha kama jina la limeorodheshwa katika orodha ya wapiga kura na baadae ataitaji mpiga kura  kuwa na kitambulisho chochote kabla ya kupiga kura ili kumtambulisha yeye ni raia wa Tanzania.
“Ikiwa Mpiga kura hatakuwa na kitambulisho cha aina yeyote lakini jina lake likaonekana katika orodha ya wapiga kura iliyoandaliwa kwa mujibu wa kanuni za uchaguzi,Msimamizi huyo atamruhusu kupiga kura baada ya kutambuliwa na wakazi wa eneo hilo,”alisema Sagin
Akizungumzia katika Mikoa iliyofanya vizuri katika uandikishwa wa wapiga kura  Sagin alisema Dar es Salaam ni miongoni mwa mikoa iliyofanya vibaya katika zoezi hilo ikiwa na asilimia 43,halmashauri ya Wilaya ya Kilindi 21,Same 22.
Akizitaja Halmashauri zilizofanya vizuri ni Katavi asilimia 79, Kagera 78, Kilimanjaro 50, katavi 107,Babati 101.
Pia Sagin alisema kuwa siku ya jumapili Disemba 14  wapiga kura waliojiandikisha katika daftari la kupiga kura ni 11,491,661 ambao wanatarajiwa kupiga na kusisitiza kuwa wananchi  kujitokeza kupiga kura bila hofu ya usalama.


No comments:

Post a Comment